Polisi Watakiwa Kuongeza Kasi Ya Ukusanyaji Mapato
HomeHabari

Polisi Watakiwa Kuongeza Kasi Ya Ukusanyaji Mapato

Na. A/INSP Frank Lukwaro- Jeshi la Polisi. Mkutano wa Maafisa Wanandhimu, Wakuu wa Usalama barabarani na Wahasibu wa Polisi kutoka mikoa...


Na. A/INSP Frank Lukwaro- Jeshi la Polisi.

Mkutano wa Maafisa Wanandhimu, Wakuu wa Usalama barabarani na Wahasibu wa Polisi kutoka mikoa yote Tanzania bara na Zanzibar wametakiwa kuongeza kasi katika kukusanya maduhuli ya serikali ikiwemo kuwasimia walio chini yao ili kuepusha hoja za kiukaguzi ambazo zinaweza kujitokeza kutokana na usimamizi usioridhisha kwa baadhi ya Viongozi.

Hayo yamesemwa na Kamishna wa Fedha na Lojistiki Hamad Hamis Hamad wakati wa siku ya pili ya mkutano huo unaoendelea Mkoani Kilimanjaro kwa lengo la kuboresha utendaji kazi kwa washiriki hao pamoja na kujiimarisha katika utumiaji mifumo ya kidigitali katika kukusanya mapato ya serikali ikiwemo tozo za barabarani.

Amesema ni vizuri washiriki wa mkutano huo kuhakikisha kuwa mkutano huo utakapomalizika mabadiliko yaweze kuonekana kwa vitendo kwakuwa kila mmoja anatakiwa kutambua wajibu wake katika kuhakikisha kuwa mapato ya Serikali yanakusanywa na kufikishwa katika mamlaka husika kwa wakati.

“Kila mmoja aone umuhimu wa kuongeza bidii katika ukusanyaji wa mapato na kuimarisha usimamizi wa matumizi ya fedha na rasilimali za umma ili kufikia malengo ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania” Alisema Kamishna Hamad.

Mkutano huo pia umeshirikisha wadau wa nje wakiwemo Wizara ya Fedha na Mipango, Mamlaka ya udhibiti wa Ardhini (LATRA), Ofisi ya Mhakiki mali wa Serikali ambapo wameweza kuwasilisha mada zao na kufanya majadiliano ya pamoja ili kuboresha ushirikiano uliopo baina ya taasisi hizo na Serikali.

Vilevile Wajumbe hao wameweza kuelimishwa kuhusu ufanyaji kazi wa mashine mpya za ukusanyaji wa tozo za serikali (POS) ambapo zimeboreshwa katika ufanyanyaji wa kazi ambapo jumla ya mashine hizo 2,050 zimenunuliwa ili kuendeleza zoezi hilo la ukusanyaji wa tozo hususani za barabarani.

Mkutano huo ulifunguliwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na unatarajia kufungwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini unabebwa na kauli mbiu ya Kusanya mapato, Simamia fedha na mal iza Umma kwa maendeleo ya Taifa.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Polisi Watakiwa Kuongeza Kasi Ya Ukusanyaji Mapato
Polisi Watakiwa Kuongeza Kasi Ya Ukusanyaji Mapato
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEj9lh12z-20dkmrp-EgBcgXyGNTD4wGnYMliMGNuosdT_cDoCgatuks-_A1roCYJ745bCMb3Lo9-FA4sVxyFDWHy6zclm7dV8WLx6ws6V2NeUdWpN_b1iz5tdTVHxEEdLdCp2YnFA4QtOoN61tcfqklHZ7o73TiugdrpNATnqT8AF-HX7oKGIoUj6v0rA=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEj9lh12z-20dkmrp-EgBcgXyGNTD4wGnYMliMGNuosdT_cDoCgatuks-_A1roCYJ745bCMb3Lo9-FA4sVxyFDWHy6zclm7dV8WLx6ws6V2NeUdWpN_b1iz5tdTVHxEEdLdCp2YnFA4QtOoN61tcfqklHZ7o73TiugdrpNATnqT8AF-HX7oKGIoUj6v0rA=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/11/polisi-watakiwa-kuongeza-kasi-ya.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/11/polisi-watakiwa-kuongeza-kasi-ya.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy