Halmashauri Momba Yaikatisha Tamaa NHC Kujenga Nyumba Za Watumishi Songwe
HomeHabari

Halmashauri Momba Yaikatisha Tamaa NHC Kujenga Nyumba Za Watumishi Songwe

Na Munir Shemweta, WANMM SONGWE Deni la shilingi milioni 384,875,921.01 inalodaiwa Halmashauri ya wilaya ya Momba mkoa wa Songwe na Shir...

Bunge Live: Bunge La 12 Mkutano Wa 3 Kikao Cha 8 Tarehe 13.04.2021
Bunge Lapitisha Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 hadi 2025/26.
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo April 13


Na Munir Shemweta, WANMM SONGWE
Deni la shilingi milioni 384,875,921.01 inalodaiwa Halmashauri ya wilaya ya Momba mkoa wa Songwe na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kwa kuijengea nyumba ishirini za watumishi limelikatisha tamaa shirika hilo kujenga nyumba katika halmashauri za mkoa huo kwa hofu ya kutokulipwa fedha.

Hayo yamebainika wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula tarehe 22 Februari 2021 alipotembelea mkoa wa Songwe kukagua utendaji kazi wa sekta ya ardhi na kuhamasisha ulipaji kodi ya pango la ardhi katika mko huo.

Mkuu wa mkoa wa Songwe Brigedia Jenerali Nicodemus Mwengela wakati wa kikao baina ya Naibu Waziri wa Ardhi Dkt Angeline Mabula na Watendaji wa sekta ya ardhi aliliomba Shirika la Nyumba la Taifa kujenga nyumba katika halmashauri za mkoa wa Songwe na kuziuzia halmashauri  ili kupunguza  uhaba wa nyumba za watumishi.

‘’Ni vizuri sasa Shirika la Nyumba la Taifa likaangalia namna ya kujenga nyumba katika halmashauri za mkoa wa Songwe ili kuopunguza uhaba wa nyumba kwa watumishi’’ alisema Brigedia Jenerali Mwengela.

Meneja Huduma kwa Huduma kwa Jamii wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Bw. Muungano Saguya alisema Shirika lake mbali na kufanya kazi ya upangaji miji katika maeneo mbalimbali  limekuwa likijenga nyumba na kuziuzia halmashauri kwa makubalianio ya kulipa kwa awamu  na kutolea mfano wa ujenzi wa nyumba katika halmashauri za Uyui na Busekelo.

Hata hivyo, alisema katika kutekeleza azma Shirika limekumbana na changamoto katika  halmashauri ya wilaya ya Momba mkoa wa Songwe ambapo halmashauri hiyo imeshindwa  kulipa deni lake la Shilingi milioni 384.8 kwa wakati kama ilivyoahidi katika barua yake ya tarehe 5 Novemba 2019 na kulifanya shirika kutafakari namna ya kuendelea na miradi ya aina hiyo katika mkoa wa Songwe.

Akizungumzia suala hilo, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula aliitaka halmashauri ya Momba kuhakikisha inalipa deni hilo haraka ili kulifanya shirika kuacha kutumia fedha zake kutekeleza miradi hiyo.

‘’Shirika la Nyumba la Taifa likiendelea kutumia fedha zake kutekeleza miradi litashindwa kutekeleza majukumu yake’’ alisema Naibu Waziri Mabula.

Alisema, kwa sasa Shirika la Nyumba la Taifa linajenga nyumba kulingana na mahitaji ya mteja na lengo kubwa ni kuwawezesha watumishi kuweza kuishi katika nyumba bora na kusisitiza kuwa halmashauri zinatakiwa kuingia mikataba ya ujenzi wa nyumba na NHC  ambapo alisema nyumba hizo ni vitega uchumi vya halmashauri.

Mkuu wa Wilaya ya Momba Juma Irando aliahidi kukaa na Shirika la nyumba la Taifa (NHC) kungalia namna bora ya kuharakisha kulipa deni la halmashauri hiyo ili kuondoa hofu kwa shirika kujenga nyumba za watumishi katika halmashauri za mkoa wa Songwe.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Momba Adrean Jungu aliahidi halmashauri yake kulipa deni hilo haraka katika kipindi cha mwaka huu wa fedha ili kujenga imani kwa Shirika kwa halmashauri nyingine za mkoa huo


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Halmashauri Momba Yaikatisha Tamaa NHC Kujenga Nyumba Za Watumishi Songwe
Halmashauri Momba Yaikatisha Tamaa NHC Kujenga Nyumba Za Watumishi Songwe
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg1hQyM4YS8kFbf3ShXbcPFrTKa4qGZ0AXuknZFWpY4Wo_MelO101xa0QUTfLyTEB5lmr46PLvD51wR0GqXNul8FxIqLTz2xO6jzrutSyrsERhqkF7gjP1buVEhi54LIrxR5pusAs-vr45q/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg1hQyM4YS8kFbf3ShXbcPFrTKa4qGZ0AXuknZFWpY4Wo_MelO101xa0QUTfLyTEB5lmr46PLvD51wR0GqXNul8FxIqLTz2xO6jzrutSyrsERhqkF7gjP1buVEhi54LIrxR5pusAs-vr45q/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/halmashauri-momba-yaikatisha-tamaa-nhc.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/halmashauri-momba-yaikatisha-tamaa-nhc.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy