Ole Nasha Akutana Na Spika Wa Bunge La Afrika Mashariki
HomeHabari

Ole Nasha Akutana Na Spika Wa Bunge La Afrika Mashariki

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. William Ole Nasha (Mb.) amekutana na kufanya mazungumzo na Spika wa ...

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo January 18, 2024
Waziri wa usalama wa taifa Israel atishia kujiuzulu ikiwa watakubali kusitisha mapigano
Mahakama ya Korea Kusini yakataa ombi linalopinga kuwekwa kizuizini kwa Yoon


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. William Ole Nasha (Mb.) amekutana na kufanya mazungumzo na Spika wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Martin K. Ngoga ofisini kwake jijini Dodoma tarehe 26 Januari, 2021.

Viongozi hao wamejadili namna watakavyoimarisha uhusiano baina ya Tanzania na Bunge hilo la Afrika Mashariki na kuliwezesha Bunge hilo kutekeleza majukumu yake kikamilifu huku likizingatia sheria, kanuni , taratibu na uadilifu.

 Akizungumza katika kikao hicho Naibu Waziri Ole Nasha amemtaarifu Spika huyo wa Bunge la Afrika Mashariki kwamba Tanzania imekua ikifanya juhudi kubwa katika kuhakikisha nchi za Afrika ikiwemo Jumuiya ya Afrika Mashariki zinaimarisha mtangamano na kuongeza kwamba Bunge hilo la Afrika Mashariki ni moja kati ya vyombo muhimu sana katika Jumuiya ya Afrika Mashariki vinavyoimarisha mtangamano.

Amemuomba Mhe. Spika kuendelea kulisimamia Bunge hilo kwa kufuata Mkataba ulioanzisha Jumuiya ya Afrika Mashariki, Itifaki na Kanuni za Jumuiya ili kuzingatia utawala bora.

Mhe. Naibu Waziri amemkumbusha Spika huyo kwamba Bunge la Afrika Mashariki ni chombo kinachoziangalia taasisi za Jumuiya hivyo lazima kiwe chombo cha mfano kwa Serikali za nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika uendeshaji wa shughuli zake na kuzingatia weledi.

Akizungumzia kuhusu bajeti ya Jumuiya kwa mwaka wa fedha 2020/2021, Mhe. Naibu Waziri alimtakia heri katika kupitisha Bajeti hiyo kwenye Mkutano wa Bunge hilo utakaofanyika mwanzoni mwa mwezi Februari, 2021.

Naye Mhe. Spika Ngoga ameshukuru kwa maoni na msimamo wa Tanzania katika masuala mbalimbali ndani ya Jumuiya na kuelezea masikitiko yake baada ya Bunge kushindwa kupitisha Bajeti iliyowasilishwa na Baraza la Mawaziri la Jumuiya.

Ameahidi kuyafanyia kazi maoni ambayo ameyapokea kutoka kwa nchi wanachama ikiwamo Tanzania kwa ajili ya manufaa ya nchi hizo na wananchi wake na kuongeza kuwa atatumia uzoefu wake kuhakikisha Bajeti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki inapitishwa na Bunge ili shughuli za Jumuiya ziendelee.


 



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Ole Nasha Akutana Na Spika Wa Bunge La Afrika Mashariki
Ole Nasha Akutana Na Spika Wa Bunge La Afrika Mashariki
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiOKxnd-LOIVznBxqlMCVH0yojikxR7FlLjgMJg2bl3Wc9aYTVLD56FYC1mqGk3W3bSYF8NeVcndxldKLDuzVMdVDYoKvgEz0RtC_bLXjySVZ4guzebvRijb8Z59sxUhwLxMN-foe3HQLYq/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiOKxnd-LOIVznBxqlMCVH0yojikxR7FlLjgMJg2bl3Wc9aYTVLD56FYC1mqGk3W3bSYF8NeVcndxldKLDuzVMdVDYoKvgEz0RtC_bLXjySVZ4guzebvRijb8Z59sxUhwLxMN-foe3HQLYq/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/01/ole-nasha-akutana-na-spika-wa-bunge-la.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/01/ole-nasha-akutana-na-spika-wa-bunge-la.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy