MWANAFUNZI ATEKWA, AUAWA
HomeMatukio

MWANAFUNZI ATEKWA, AUAWA

Na Waandishi Wetu DUNIA imekwisha jamani! Mwanafunzi wa kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari ya Mabibo, Dar, Irene Said (15) ametekw...

Runaway ostrich races onto highway in Zhejiang
Krismas Nyama Yawa patashika
Leading Women's most inspiring women of 2014

Na Waandishi Wetu
DUNIA imekwisha jamani! Mwanafunzi wa kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari ya Mabibo, Dar, Irene Said (15) ametekwa, amebakwa na kuuawa kikatili kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili huku ikidaiwa kuwa, kijana mmoja asiyejulikana alifika nyumbani kwao, Kigogo Luhanga na kutaka kiroba na mtu mmoja waongozane akabebe ndizi.

Polisi wakiwa wamebeba mwili wa marehemu.

Akizungumzia tukio hilo la kusikitisha sana, mama mdogo wa marehemu, Doto Lucas alisema:
“Siku ya tukio ambayo ni Alhamisi iliyopita (Machi 12), kijana mmoja ambaye hakuna aliyemfahamu alikuja hapa nyumbani na kumtaka mtu mmoja na kiroba ili akachukue ndizi ambazo kuna mtu aliagiza ziletwe.

“Marehemu ndiye aliyekuwa karibu akijisomea baada ya kutoka shuleni. Mtu mkubwa aliyekuwa nyumbani muda huo ni bibi wa marehemu ambaye ni mtu mzima hivyo alimwambia Irene aongozane na mtu huyo akachukue mzigo akijua uko jirani kwa mujibu wa mtu huyo.

“Baada ya muda, yule kijana alirudi akiwa peke yake na kusema anataka chombo kingine cha kubebea kwa kuwa kile kiroba kilikuwa hakitoshi.“Bibi mtu alimuonesha ndoo kwa vile hakukuwa na kiroba kingine, alipoitwaa na kuondoka nayo ndiyo hakurudi yeye wala Irene.Wanafunzi wenzake wakiwa na majonzi msibani.

“Baada ya kuona muda unayoyoma bibi wa marehemu alianza kupata wasiwasi. Ndipo akatutaarifu kilichotokea nyumbani na sisi tukaanza kumsaka Irene na kijana yule.”

KWA NINI WALIMWAMINI KIJANA HUYO?
“Sisi tuna makaka zetu wakubwa ambao wana kawaida ya kutuagizia mizigo mbalimbali kwenye magari, kwa hiyo tuliamini ni wao. Lakini tulipowapigia simu na kuwaeleza tukio hilo wote walikanusha kuwa si wao na kushangaa.

“Kauli hiyo ilianza kututia shaka zaidi hivyo tulianza kuwasiliana na ndugu na jamaa ambao wote waliishia kushangaa. Tukaenda kutoa taarifa Kituo cha Polisi, Kigogo na kuanza msako wa kumsaka binti yetu pamoja na mtuhumiwa.”

Gari la polisi likiwa eneo la tukio.

IRENE APATIKANA AKIWA AMEUAWA
Mwanamke huyo anaendelea kusimulia: “Kesho yake asubuhi (Ijumaa) tukasikia kuna binti amekutwa ameuawa kinyama kwenye Bonde la Mto Msimbazi, eneo la Sukita. Tulipatwa na mshituko, tukaenda na kuukuta mwili, tulipoukagua tuligundua ni Irene.

“Alikuwa ameharibiwa vibaya. Sehemu za mwii alikuwa na damu, alichomwa na kitu chenye ncha kali. Kwa vyovyote yule kijana alikuwa na wenzake, walimteka huko mbele ya safari na kumbaka kabla ya kumuua. Inauma sana jamani.”

Marehemu Irene ambaye katika mazishi yake wanafunzi wenzake walikuwa wakilia sana, alizikwa Jumamosi iliyopita katika Makaburi ya Mburahati, Dar.

Wanafunzi wenzake wakiaga mwili wa mpendwa wao.

Katika ibada hiyo, Katekista aliyesaidiana na paroko kuendesha ibada hiyo aliyetajwa kwa jina moja la Henjewele aliwalaani vikali walioshiriki kufanya unyama huo na kuwataka wafanye toba haraka iwezekanavyo na kumrudia Mungu wao vinginevyo laana na moto wa milele utawaangukia.
Mungu ailaze roho ya marehemu Irene mahali pema peponi- Amina.
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: MWANAFUNZI ATEKWA, AUAWA
MWANAFUNZI ATEKWA, AUAWA
http://api.ning.com/files/EFRV*I*wRwLO6VB1VFlx97ZE2VTx2GjjLnz7pzn7CQlEgUYPAhhEYeaPtIZJbVVIWJPAs*RbXAPwT5fVF26PLFa9jxZtTFJ5/21.jpg?width=650
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/03/mwanafunzi-atekwa-auawa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/03/mwanafunzi-atekwa-auawa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy