Kikosi cha Yanga ya Dar es Salaam Timu ya Yanga ya jijini Dar es salaam hapo jana ilifan...
Timu ya Yanga ya jijini Dar es salaam hapo jana ilifanikiwa kutinga hatua ya Robo Fainali ya Mashindano ya Kombe la Mapinduzi huko Visiwani Zanzibar baada ya kuitandika Polisi ya Zanzibar mabao 4-0 kwenye Mechi ya Kundi A.
Ushindi huu ni wa pili kwa Yanga kwenye Kundi lao baada ya kuichapa Taifa ya Jang’ombe magoli 4-0 katika Mechi yao ya kwanza na sasa wanaongoza Kundi A wakiwa na alama 6.
Hadi Mapumziko Yanga walikuwa mbele kwa mabao 2-0 ya Mchezaji wa Brazil Coutinho na yule wa Liberia Kpah Sherman.
Kipindi cha Pili Yanga walipiga Bao nyingine 2 kupitia Coutinho na Simon Msuva.
Katika Mechi nyingine zilizopigwa Jana Usiku, Azam FC iliichapa KMKM Bao 1-0 katika Mechi ya Kundi B na kupata ushindi wao wa kwanza baada ya kutoka 2-2 na KCCA ya Uganda katika Mechi yao ya kwanza.
Huku nao mabingwa wa kombe hilo Timu ya KCCA ya uganda wakifanikiwa kusonga mbele baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Timu ya Mtende ya Zanzibar
Mashindano hayo yanaendelea tena leo huko Visiwani Zanzibar kwa Mechi mbili katika uwanja wa Amani,Mechi ya kwanza ni kati ya Mtibwa Sugar na Mafunzo ikifuafuatiwa na mechi ya Simba dhidi ya Timu ya JKU
COMMENTS