Watumishi Wajengewa Uwezo Kuhusu Mradi Wa Tanzania Ya Kidijitali
HomeHabari

Watumishi Wajengewa Uwezo Kuhusu Mradi Wa Tanzania Ya Kidijitali

  Mratibu wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bwana Honest Njau ameuzungumzi...

Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo November 18, 2024
Ajali mbaya yatokea Geita usiku wa kuamkia leo
Habari kubwa Magazetini Kenya leo November 17, 2024


 Mratibu wa Mradi wa Tanzania ya Kidijitali kutoka Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bwana Honest Njau ameuzungumzia mradi huo kuwa ni mradi wa kimapinduzi unaoenda kuboresha na kuongeza matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika shughuli za uzalishaji pamoja na kutoa au kupokea huduma za Serikali na zile za kijamii na kiuchumi

Akizungumza wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi wa Wizara hiyo yanayofanyika jijini Arusha, Bwana Njau amesema kuwa ili kuweza kuwa na mabalozi wazuri ni vema kila mtumishi kufahamu kinachoenda kufanyika kupitia mradi huo ili kufikia uchumi wa kidijitali

“Tayari tupo kwenye zama za kidijitali, kinachofanyika kupitia mradi huu ni kuboresha zaidi kwa kuchangia kuongeza wigo wa kutoa huduma za Serikali kwa wananchi, kuboresha huduma za mawasiliano na kuhakikisha Taifa linakuwa na wataalamu weledi na wabunifu wa kutosha wa TEHAMA ili kuweza kusimamia mabadiliko ya kidijitali yanayoendelea kufanyika nchini na duniani kote”, amezungumza Njau

Ameongeza kuwa kupitia mradi huo Serikali inakwenda kuboresha miundombinu na maeneo mahususi ya uchumi ili kuendana na uchumi wa Kidijitali ikiwa ni pamoja na kuwezesha biashara mtandao kwa kutengeneza platform kubwa ya biashara itakayoiunganisha nchi na dunia

“Tunaposema majukwaa(platforms) ya biashara mtandao haimaanishi mitandao ya kijamii pekee ila ni pamoja na kuwa na majukwaa mengine ya kufanya biashara mtandao kwa mfano Sarafu ya Azam Bakhresa, Alibaba, Kikuu na mingine mingi kama hiyo, hivyo kama nchi tunatakiwa kuwa na platform kubwa itakayotuunganisha na dunia”, amefafanua Njau

Katika hatua nyingine, watumishi hao wamepitishwa katika mada ya matumizi salama ya mtandao ambapo, Mkurugenzi Msaidizi anayeshughulikia masuala ya Usalama Mtandao wa Wizara hiyo, Mhandisi Steven Wangwe aliyetoa mada hiyo kwa njia ya mtandao ameangazia sheria yenyewe ya makosa ya mtandao ya mwaka 2015 na makosa yake yanayoweza kutokea kwa kukiuka usiri, uadilifu na upatikanaji wa taarifa.

Mhandisi Wangwe ameyabainisha makosa yanayofanyika kwa njia ya mtandao ni pamoja na usambazaji wa taarifa isivyo kwa usahihi, udhalilishaji wa mtandao, kutoa taarifa za uongo, utapeli kwa kutumia vifaa vya kielektroniki kama simu na kompyuta, usambazaji wa picha za utupu na faragha kwenye mitandao, kutuma barua pepe au meseji za vitisho pamoja na udukuzi wa taarifa.

Amesema kuwa Serikali inaendelea kuhakikisha kunakuwa na matumizi salama ya mtandao kwa kutunga na kusimamia Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015 inayoainisha makosa ya kimtandao na adhabu zake ambazo ni pamoja na faini, kifungo au vyote kwa pamoja kulingana na aina ya kosa husika.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Watumishi Wajengewa Uwezo Kuhusu Mradi Wa Tanzania Ya Kidijitali
Watumishi Wajengewa Uwezo Kuhusu Mradi Wa Tanzania Ya Kidijitali
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjyZ1w2K_KciNY0Wk5_rSvd_WemDTF-nr3okKhUAEuGG3mriJrrasWF0-DIWMHG7o95JMWgCuuanw5c3OCv4gffw_zGRo4DpydYx5IgniCVn0dcVQcUyeLR1xnzzItr8rtlNL1JzMpDMBU9rQgA9VDTM0kcoYJWqitnUkdfdWCOgF7NZZH35koR7Hghbw/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjyZ1w2K_KciNY0Wk5_rSvd_WemDTF-nr3okKhUAEuGG3mriJrrasWF0-DIWMHG7o95JMWgCuuanw5c3OCv4gffw_zGRo4DpydYx5IgniCVn0dcVQcUyeLR1xnzzItr8rtlNL1JzMpDMBU9rQgA9VDTM0kcoYJWqitnUkdfdWCOgF7NZZH35koR7Hghbw/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/06/watumishi-wajengewa-uwezo-kuhusu-mradi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/06/watumishi-wajengewa-uwezo-kuhusu-mradi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy