Marekani, Norway, Uingereza na Umoja wa Ulaya zimeonya jeshi la Sudan dhidi ya kumteua waziri wao mkuu, zikisema kuwa hatua hiyo inaweza ...
Marekani, Norway, Uingereza na Umoja wa Ulaya zimeonya jeshi la Sudan dhidi ya kumteua waziri wao mkuu, zikisema kuwa hatua hiyo inaweza kulitumbukiza taifa hilo kwenye mzozo.
Nchi hizo zilisema hazitaunga mkono waziri mkuu au serikali iliyoteuliwa bila kushirikisha wadau mbalimbali wa kiraia.
Waziri mkuu wa zamani, Abdalla Hamdok, alijiuzulu siku ya Jumapili huku kukiwa na mkwamo wa kisiasa na maandamano makubwa yaliyotokana na mapinduzi ya kijeshi ya Oktoba.
Kwa mara nyingine tena nchi za Magharibi zimekemea hatua za jeshi dhidi ya waandamanaji - zaidi ya 50 wameuawa tangu mapinduzi.
Siku ya Jumanne, vikosi vya usalama vilirusha gesi ya kutoa machozi katika miji kadhaa kutawanya umati mkubwa wa watu waliokuwa wakiandamana kupinga utawala wa kijeshi
Credit: MPEKUZI
Thanks for your time please share with your friends
COMMENTS