Waziri Mchengerwa : Sitowasaliti Watumishi Wanaochapa Kazi Kwa Bidii, Weledi Na Uadilifu
HomeHabari

Waziri Mchengerwa : Sitowasaliti Watumishi Wanaochapa Kazi Kwa Bidii, Weledi Na Uadilifu

Na. James K. Mwanamyoto-Kigoma Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa a...

Serikali kufutia leseni kwa wanaopandisha bei ya mafuta ya kupikia
Ndugulile Ajikita Kutatua Changamoto Za Mawasiliano Ya Simu Na Data
Biden na Putin wajadili mahusiano ya Urus na Marekani


Na. James K. Mwanamyoto-Kigoma
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema katika uongozi wake hatowasaliti katika kutetea stahiki zao Watumishi wa Umma wanaofanya kazi kwa bidii, weledi, uadilifu na uzalendo kwa taifa lao.

Akizungumza na Viongozi na Watumishi wa Umma wa Mkoa wa Kigoma, Mhe. Mchengerwa amesema atahakikisha anasimamia haki na stahiki za Watumishi wa Umma nchini kwa lengo la kuwaongezea morali ya utendaji kazi kama ambavyo Serikali ya Awamu ya Sita imekusudia.

Kufuatia uamuzi wake wa kusimamia haki na stahiki za Watumishi wa Umma, Mhe. Mchengerwa ametoa rai kwa watumishi wote wa umma nchini kufanya kazi kwa bidii na uadilifu ili kuendana na kasi ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan badala ya kufanya kazi kwa mazoea kwani wasipowajibika hatokuwa tayari kutetea stahiki zao.

“Pale ambapo tutabaini kuna mtumishi mzembe, mla rushwa na mbadhirifu wa mali za umma sitokuwa tayari kumtetea lakini nitakuwa tayari kupambana na kumtetea mtumishi yeyote mwadilifu, mchapakazi na mzalendo kwa taifa lake muda wote asubuhi, mchana, jioni na usiku,” Mhe. Mchengerwa amesisitiza.

Mhe. Mchengerwa amewaelekeza watendaji kufuatilia utendaji kazi wa watumishi walio chini yao mara kwa mara na kumtaka kila mtumishi kuongeza ubunifu katika eneo lake la kazi ili aweze kutoa huduma bora kwa wananchi ambao ndio walengwa wakuu wa huduma zinazotolewa na taasisi za umma nchini.

Aidha, Mhe. Mchengerwa amewataka waajiri kutenga bajeti ya mafunzo kwa ajili ya kuwajengea uwezo wa kiutendaji Watumishi wa Umma walio katika maeneo yao ili waweze kuwa na weledi, ubunifu na kuongeza ufanisi kiutendaji.

Waziri Mchengerwa yuko kwenye ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani Kigoma yenye lengo la kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wa umma na kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi wa umma mkoani humo.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Waziri Mchengerwa : Sitowasaliti Watumishi Wanaochapa Kazi Kwa Bidii, Weledi Na Uadilifu
Waziri Mchengerwa : Sitowasaliti Watumishi Wanaochapa Kazi Kwa Bidii, Weledi Na Uadilifu
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhMS4ppvl1hvRMafuUqplo6lepY4-K5Xxc-_t8nNdwUqw87oL51bfjncrMgMrpPS0NTNus-TvJ_DuuYuqOEZAUWm4INmbkWNkCq0cu3NqoSx01g3R1paQFK73-2nJKD2x_GG_IVakOIh62u8OHmK1uMUNZzIj6TccTRjLvyHwndVicT4aipEpXeOsKGiA=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhMS4ppvl1hvRMafuUqplo6lepY4-K5Xxc-_t8nNdwUqw87oL51bfjncrMgMrpPS0NTNus-TvJ_DuuYuqOEZAUWm4INmbkWNkCq0cu3NqoSx01g3R1paQFK73-2nJKD2x_GG_IVakOIh62u8OHmK1uMUNZzIj6TccTRjLvyHwndVicT4aipEpXeOsKGiA=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/waziri-mchengerwa-sitowasaliti.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/waziri-mchengerwa-sitowasaliti.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy