Mabadiliko Ya Tabia Nchi Kudhibitiwa, Kuinua Uchumi Wa Buluu
HomeHabari

Mabadiliko Ya Tabia Nchi Kudhibitiwa, Kuinua Uchumi Wa Buluu

  Na. Edward Kondela Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (Mb), amesema Tanzania ni moja ya nchi kusini mwa janga la sahara amb...

Waziri Kijaji: Tanzania Itaendeleza Ushirikiano Wa Kibiashara Kati Ya Tanzania Na Uingereza
Tanzania Kuwavutia Wawekezaji Kwenye Siku Ya Tanzania Maonesho Ya Expo 2020 Dubai
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo February 2

 


Na. Edward Kondela
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (Mb), amesema Tanzania ni moja ya nchi kusini mwa janga la sahara ambayo inaweka mikakati ya namna ya kudhibiti mabadiliko ya tabia nchi kwa kuvua kiendelevu mazao ya uvuvi yaliyopo katika Bahari ya Hindi.

Waziri Ndaki amebainisha hayo (19.11.2021) jijini Dar es Salaam mara baada ya kuhudhuria mkutano wa kimataifa kwa njia ya video, kuhusu uchumi wa buluu ambao umefanyika Mjini Maputo nchini Msumbiji na kubainisha kuwa mkutano umejadili namna nchi zinazozunguka Bahari ya Hindi na kusini mwa janga la sahara zinavyoweza kudhibiti mabadiliko ya tabia nchi.

Amebainisha kuwa mkutano huo umeangalia namna nchi hizo zinavyoweza kudhibiti mabadiliko ya tabia nchi kwa kuvua kiendelevu na kutoharibu mazingira hali inayoweza kusababisha mabadiliko ya tabia nchi na kusababisha madhara katika sekta ya uvuvi.

Aidha, amesema mkutano huo umejadili mambo mbalimbali kuhusu uwekezaji wa uchumi wa buluu katika nchi ambazo zinazunguka Bahari ya Hindi na kusini mwa janga la sahara ambapo amefafanua kuwa uwekezaji bado ni tatizo hasa rasilimali fedha kwa nchi zinazoendelea.

Pia ameongeza kuwa mkutano huo umeangalia uvunaji wa rasilimali za mazao ya uvuvi katika Bahari ya Hindi kiendelevu pamoja na kudhibiti uvuvi haramu kwa kuweka mikakati mbalimbali ili uchumi wa buluu uwe na manufaa.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Nazael Madalla akizungumzia mkutano huo amesema, serikali ina mpango mkubwa wa kujenga vituo vya ukuzaji viumbe maji katika Ukanda wa Pwani pamoja na vituo vingine ili kufungua fursa ya uchumi wa bahari katika ukuzaji viumbe maji.


Dkt. Madalla ametoa wito kwa wadau mbalimbali kuanza kufikiria namna ya kuwekeza katika uchumi wa buluu ambao unahusisha shughuli mbalimbali zinazofanyika kwenye bahari, maziwa na mito.


Naye Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) Dkt. Ishmael Kimirei amesema ili uwekezaji katika uchumi wa buluu uwe na tija na kuonekana kwa fursa mbalimbali utafiti ni eneo muhimu katika kufikia manufaa hayo.

Amesema TAFIRI itafanya utafiti katika bahari kuu kuangalia wingi na mtawanyo wa samaki ili kufahamu ni maeneo gani ambayo wavuvi wanaweza kwenda kuvua na hata kufahamu mazao wanayoenda kuvua.

Mkutano wa kimataifa kuhusu uchumi wa buluu umefanyika Mjini Maputo nchini Msumbiji, ambapo kwa Tanzania Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (Mb) ameongoza ujumbe wa Tanzania kuhudhuria mkutano huo kwa njia ya video jijini Dar es salaam, ambapo mkutano umehusisha nchi zinazozunguka Bahari ya Hindi na kusini mwa janga la sahara.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Mabadiliko Ya Tabia Nchi Kudhibitiwa, Kuinua Uchumi Wa Buluu
Mabadiliko Ya Tabia Nchi Kudhibitiwa, Kuinua Uchumi Wa Buluu
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgQqmpuG_z3VcDN6ky01Bkb5oCxodfxLH0QbKgf_8tQkar0uuw3tgHCYoHgWgp_bbeDj4oFXFRKTlQYzpVF3y2qTb8zJLNK77QAb_H5wBWs-J8QdS66Z8omgwcbhmMjqCSKzAcMG84FOgdpZxMW73EWCIIWK2ZnOqsprru0mK5T5S2e2LIcN_Wxu5W-xA=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgQqmpuG_z3VcDN6ky01Bkb5oCxodfxLH0QbKgf_8tQkar0uuw3tgHCYoHgWgp_bbeDj4oFXFRKTlQYzpVF3y2qTb8zJLNK77QAb_H5wBWs-J8QdS66Z8omgwcbhmMjqCSKzAcMG84FOgdpZxMW73EWCIIWK2ZnOqsprru0mK5T5S2e2LIcN_Wxu5W-xA=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/11/mabadiliko-ya-tabia-nchi-kudhibitiwa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/11/mabadiliko-ya-tabia-nchi-kudhibitiwa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy