Rais Samia: Tunakamilisha mchakato wa kuifanya Chato iwe mkoa
HomeHabari

Rais Samia: Tunakamilisha mchakato wa kuifanya Chato iwe mkoa

 Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema, Serikali anayoingoza inakamilisha mchakato wa kuifanya Chato kuwa Mkoa. Amesema hayo ja...

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo July 30
IGP Sirro Awataka Wananchi Msidanganywe Kuhusu Chanjo Ya Corona
Nafasi 10 za Kazi Dar es Salaam University College of Education (DUCE)


 Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema, Serikali anayoingoza inakamilisha mchakato wa kuifanya Chato kuwa Mkoa.

Amesema hayo jana Alhamisi, tarehe 14 Oktoba 2021, katika Uwanja wa Magufuli, Chato mkoani Geita katika kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru na Kumbukumbu ya kifo cha miaka 22 ya Hayati Mwalimu Julius Nyerere.

Pamoja na kuwaombea, Marais wastaafu, Benjamin Willium Mkapa na John Pombe Magufuli, Rais Samia alisema, katika kumuenzi Hayati Magufuli aliyefariki dunia 17 Machi 2021, akiwa madarakani, walimua shughuli hizo kitaifa, zifanyikie wilaya ya Chato, sehemu aliyozaliwa Hayati Magufuli.

“Tumesukumwa na uamuzi wa kuja Chato ili kumuenzi mpendwa wetu Hayati Magufuli ambaye ni mzaliwa wa Chato, aliyepapenda sana nasi tunaendeleza upendo wake. Ili kumuenzi tumeamua kuja kufanya sherehe hizi ambazo kwa kawaida hufanyika makao makuu ya mkoa,” amesema Rais Samia huku akishangiliwa.

Ametumia fursa hiyo kuwaeleza kuwa “yapo mambo ambayo Hayati Magufuli aliwaahidi wana Chato wakati wa kampeni. Mambo hayo ni upanuzi wa Bandari ya Nyamilembe, kumamilisha Uwanja wa Ndege wa Chato, Hospitali ya Kanda ya Chato, Chuo cha Veta na mimi niwaahidi yote yatatekelezwa.”

Huku shangwe zikitawala uwanjani hapo, Rais Samia akasema, lipo jambo ambalo wananchi wa Chato wangependa kulisikia kutoka kwake. Kauli hiyo ilizidisha shangwe zaidi na yeye akasema “Serikali inakamilisha vigezo vinavyoruhusu Chato kuwa Mkoa. Kuna vigezo kadhaa ambavyo bado tunaendelea kuviangalia na vigezo hivi vikikidhi tunakwenda kulimaliza jambo hili.”


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Rais Samia: Tunakamilisha mchakato wa kuifanya Chato iwe mkoa
Rais Samia: Tunakamilisha mchakato wa kuifanya Chato iwe mkoa
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEjQxiM39TTbM7WBXNjFkq3HIg0wMgNbI6DhAGspaMsPCfYhC7sww-WhLEoiiQu0wgp72gRTNtIeiL_jznZrj4Hug6v3nlxhiFtC1PfeMRVXdEYOdRxKH6MoCYo-viTsMB_W1iPc3fD1cG4fWsikip4Jy9leNArlEZleJhkYszUafvHR6MGeHSkY_8Q_XQ=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEjQxiM39TTbM7WBXNjFkq3HIg0wMgNbI6DhAGspaMsPCfYhC7sww-WhLEoiiQu0wgp72gRTNtIeiL_jznZrj4Hug6v3nlxhiFtC1PfeMRVXdEYOdRxKH6MoCYo-viTsMB_W1iPc3fD1cG4fWsikip4Jy9leNArlEZleJhkYszUafvHR6MGeHSkY_8Q_XQ=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/rais-samia-tunakamilisha-mchakato-wa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/rais-samia-tunakamilisha-mchakato-wa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy