NAMNA SIMBA WALIVYOPAMBANIA POINTI TATU DODOMA
HomeMichezo

NAMNA SIMBA WALIVYOPAMBANIA POINTI TATU DODOMA

  MIKIKIMIKI ya mchezo wa Ligi Kuu Bara imeendelea kwa mara nyingine tena Simba ya Didier Gomes iliibuka na ushindi wa bao 1-0 Uwanja wa J...


 MIKIKIMIKI ya mchezo wa Ligi Kuu Bara imeendelea kwa mara nyingine tena Simba ya Didier Gomes iliibuka na ushindi wa bao 1-0 Uwanja wa Jamhuri Dodoma baada ya ubao wa Uwanja wa Jamhuri kusoma Dodoma Jiji 0-1 Simba. 

Kagere jana Oktoba Mosi alifunga bao hilo akitumia pasi ya Chris Mugalu aliyetoa pasi akiwa nje ya 18 na Kagere alipachika bao hilo kwa shuti kali akiwa ndani ya 18 likamshinda mlinda mlango Hussein Masalanga.

Katika mchezo wa jana, Gomes hakuwa na namna kwa kuwa alifanya mabadiliko ya lazima mara tatu baada ya nyota Sakho kutoka nafasi yake ikachukuliwa na Rarry Bwalya,  beki Kenedy Juma naye alitoka nafasi yake ikachukuliwa na Inonga hiyo ilikiwa ni kipindi cha kwanza.

Kipindi cha pili mchezaji wao wa tatu pia aliumia ambaye ni Taddeo Lwanga baada ya kuchezewa faulo na Salmin Hoza ambaye alionyeshwa kadi ya njano.

Dodoma Jiji inayonolewa  na Kocha Mkuu, Mbwana Makata ilikamilisha dakika 90 ikiwa pungufu baada ya nyota wao Anuary Jabir kuonyeshwa kadi nyekundu dakika ya 44 kwa kumchezea faulo Kenedy Juma. 

Jitihada za Simba kusaka ushindi zilijibu kipindi cha pili baada ya Gomes kuwatumia nyota wake wote wa kazi katika safu ya ushambuliaji ikiwa ni pamoja na John Bocco, Meddie Kagere na Chris Mugalu. 
Washambuliaji hao walikuwa na moto msimu uliopita ambapo Mugalu alifunga mabao 15, Kagere alitupia mabao 13 na Bocco mabao 16.

Dodoma Jiji walikwama kutumia nafasi ambazo walizitengeneza kupitia kwa Cleophance Mkandala pamoja na Seif Karihe ambao walikuwa ni mwiba kwa mchezo wa jana.

Unakuwa ni mchezo wa kwanza Simba kushinda msimu wa 2021/22 baada ya ule wa awali kupoteza pointi mbili walipoteza pointi mbili mbele ya Biashara United. Leo kikosi cha Simba kimerejea Dar baada ya kusepa na pointi tatu kutoka Dodoma Jiji.


Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: NAMNA SIMBA WALIVYOPAMBANIA POINTI TATU DODOMA
NAMNA SIMBA WALIVYOPAMBANIA POINTI TATU DODOMA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgYIrIed5uBw3V2hSjnHixycpLMsKRocFRShNEJp4ldBPHeyhtksAKOGmQ27nlKnqjg87C0q80NYyUFyi9_2zr4d38kayTGvoDkU0kVOixKX9A-UQNdCuezeGE-CRvPPHoenfgIRd3LWtBq/w640-h426/243793298_600959394249224_8016421527950642062_n.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgYIrIed5uBw3V2hSjnHixycpLMsKRocFRShNEJp4ldBPHeyhtksAKOGmQ27nlKnqjg87C0q80NYyUFyi9_2zr4d38kayTGvoDkU0kVOixKX9A-UQNdCuezeGE-CRvPPHoenfgIRd3LWtBq/s72-w640-c-h426/243793298_600959394249224_8016421527950642062_n.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/namna-simba-walivyopambania-pointi-tatu.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/namna-simba-walivyopambania-pointi-tatu.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy