KAHATA KUSEPA MAZIMA SIMBA, KISA DAU
HomeMichezo

KAHATA KUSEPA MAZIMA SIMBA, KISA DAU

  I MEELEZWA  kuwa  kiungo mchezeshaji  wa Simba raia wa  Kenya, Francis  Kahata ameshindwa  kufikia muafaka mzuri na  timu yake katika da...


 IMEELEZWA kuwa kiungo mchezeshaji wa Simba raia wa Kenya, Francis Kahata ameshindwa kufikia muafaka mzuri na timu yake katika dau la usajili huku fasta akikwea pipa kurejea nyumbani kwao nchini Kenya.

 

Kiungo huyo juzi rasmi alimaliza mkataba wake wa miaka miwili ya kukipiga Simba aliyojiunga nayo msimu wa 2019/2020 akitokea Gor Mahia ya nchini Kenya kama mchezaji huru.

 

Nyota huyo hivi karibuni jina lake lilikatwa katika usajili wa Ligi Kuu Bara na nafasi yake kuchukuliwa na Mzimbabwe Perfect Chikwende aliyejiunga na Simba katika usajili wa dirisha dogo msimu huu.

 

Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Championi Jumatano, Simba imeshindwa kufikia muafaka mzuri wa kumuongezea mkataba baada ya kushindwana katika maslahi kwenye pande hizo mbili.

 

Mtoa taarifa huyo alisema kuwa uongozi wa Simba ulimpa mkataba aliotakiwa kusaini bure huku wakiboresha mshahara wake wa kila mwezi pekee, kitendo ambacho amekikataa kiungo huyo kabla ya juzi jioni kukwea pipa kurejea kwao.


Aliongeza kuwa upo uwezekano mkubwa wa kiungo huyo kutorejea tena kukipiga katika timu hiyo msimu ujao baada ya kushindwa kufikia muafaka mzuri.

“Kahata kaondoka tangu jana (juzi) jioni baada ya kushindwa kufikia muafaka mzuri na viongozi wa Simba kutokana na kukataa ofa aliyowekewa mezani.“Kikubwa viongozi wa Simba walitaka kumpa mkataba wa miaka miwili bila ya dau la usajili huku wakimboreshea sehemu ya mshahara wake, kitendo hicho amekikataa na kupanda ndege kurudi kwao,” alisema mtoa taarifa huyo.

 

Alipotafutwa Mkuu wa Mahudhui wa Simba, Ally Shatry kuzungumzia hilo alisema kuwa: “Sina uhakika sana hilo la kurejea nyumbani kwao Kenya.

 

“Kama amerejea kwao, basi yatakuwepo makubaliano kati ya kocha Gomes (Didier) na mchezaji mwenyewe, kwani kama unavyofahamu mchezaji huyo jina lake liliondolewa katika usajili wa ligi na badala yake kuweka katika michuano ya kimataifa.

 

“Hivyo, huenda kocha kamruhusu kurejea kwao kwa ajili ya mapumziko kwani hivi sasa hatushiriki michuano ya kimataifa, tumebakiwa na ligi na FA pekee na yeye hatumiki, kuhusiana na kuachwa sijapata taarifa rasmi kwa viongozi wangu wa juu,” alisema Shatry.



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: KAHATA KUSEPA MAZIMA SIMBA, KISA DAU
KAHATA KUSEPA MAZIMA SIMBA, KISA DAU
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiLe7ZUd3BsZbLoWqTYAzDAJAYZTOVoPLoE7TLv-4gg_7wRuxOs5YYco0gncoMFkzpTjDiasn2DaK0yJbSl5DIUsJytLKOcjxCBaeahsY9fW4Ierk0O5hr4OMGri5DIQORVU6ob1RyGG3gZ/w640-h426/Francis-Kahata.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiLe7ZUd3BsZbLoWqTYAzDAJAYZTOVoPLoE7TLv-4gg_7wRuxOs5YYco0gncoMFkzpTjDiasn2DaK0yJbSl5DIUsJytLKOcjxCBaeahsY9fW4Ierk0O5hr4OMGri5DIQORVU6ob1RyGG3gZ/s72-w640-c-h426/Francis-Kahata.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/kahata-kusepa-mazima-simba-kisa-dau.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/kahata-kusepa-mazima-simba-kisa-dau.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy