Kilimo Hai Ni Ajira Ya Uhakika Kwa Vijana
HomeHabari

Kilimo Hai Ni Ajira Ya Uhakika Kwa Vijana

Vijana nchini wameshauriwa kujiunga katika vikundi na kuanzisha mashamba yanayotumia kilimo hai kwa kulima bila kutumia kemikali ili kuwa...

NECTA Yatangaza Matokeo....Yasema ufaulu kidato cha nne umeongezeka
Breaking: NECTA Yatangaza Matokeo ya Kidato cha Nne, Darasa la Nne, Kidato cha pili
Taarifa kwa Umma Toka Idara ya Uhamiaji

Vijana nchini wameshauriwa kujiunga katika vikundi na kuanzisha mashamba yanayotumia kilimo hai kwa kulima bila kutumia kemikali ili kuwa na uhakika wa soko na kipato.

Kauli hiyo imetolewa na Mratibu wa Mkakati wa Vijana Kushiriki katika kilimo toka Wizara ya Kilimo Revelian Ngaiza jana (27.04.2021) wakati alipotembelea vikundi vya vijana wanaofanya kazi za kilimo hai kijiji cha Kalengakelu wilaya ya Mlimba Mkoa wa Morogoro.

Ngaiza aliongozana na wataalam wa shirika la Kilimo Endelevu (Sustainable Agriculture of Tanzania-SAT) alijionea mashamba ya mpunga ya vijana wa kijiji cha Kalengaleku ikiwemo vitongoji vya Nyumbanguru na Samola ambao wanazalisha mazao ya mpunga na mazao ya bustani kwa njia ya kilimo hai.

"Lengo la Wizara ya Kilimo ni kuona nguvu kazi iliyopo ya vijana takribani asilimia 58 inashiriki kwenye kazi za uzalishaji mali kupitia kilimo ili kukuza uchumi wa kaya na taifa" alisema Ngaiza

Mratibu huyo wa Mkakati wa Vijana katika kilimo alibainisha fursa zilizopo kwenye kilimo ikiwemo kilimo hai ambacho hakitumii kemikali kuwa ni uhakika wa masoko kutokana na watum wengi kupenda kutumia vyakula vilivyozalishwa bila kemikali 

Naye Mratibu wa mradi wa Kilimo Hai toka shirika la SAT  wilaya ya Mlimba Elizabeth Msobi alisema jumla ya vijana 97 kwenye kijiji cha Kalengakelu wamejiunga kwenye vikundi na wanazalisha mazao ya mpunga na bustani kwa njia ya kilimo hai (organic farming) bila kutumia kemikali au madawa kuua wadudu hivyo kutunza mazaingira na afya ya mlaji.

Msobi aliongeza kusema changamoto kubwa kwa vijanwa Mlimba ni ukosefu wa ardhi hali inayokatisha tamaa vijana wengi kujiunga hususan wanawake  .

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kikundi cha Kilimo Hai Kitongoji cha Samola kijiji cha Kalengakelu Daud  Kalinga aliomba serikali iagize viongozi wa vijiji kugawa ardhi kwa vijana.

"Serikali itupatie ardhi sisi vijana ili tulime Kilimo hai badala ya sasa tunachangishana kukodi ekari moja kwa shilingi 100,000 ni fedha nyingi mno,tunashindwa kufanya kilimo" alisema kijana Daudi.




Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Kilimo Hai Ni Ajira Ya Uhakika Kwa Vijana
Kilimo Hai Ni Ajira Ya Uhakika Kwa Vijana
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjLgQfbuhiuQzUugz6YZKkM60-9iS8gTGCipMnw-hNRlCzvMRbrBDykBxwc63tqeS8gpGQYlNoZXHH37QRVqt_KnLHw6Wf0zImX16AiuwZnAEi9x_2MOpumC3hcL912cihTKnXlq3QnQHP0/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjLgQfbuhiuQzUugz6YZKkM60-9iS8gTGCipMnw-hNRlCzvMRbrBDykBxwc63tqeS8gpGQYlNoZXHH37QRVqt_KnLHw6Wf0zImX16AiuwZnAEi9x_2MOpumC3hcL912cihTKnXlq3QnQHP0/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/04/kilimo-hai-ni-ajira-ya-uhakika-kwa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/04/kilimo-hai-ni-ajira-ya-uhakika-kwa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy