UONGOZI wa Yanga umesema kuwa malengo yao makubwa ni kuweza kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara jambo wanaloamini kwamba litatimia. Kweny...
UONGOZI wa Yanga umesema kuwa malengo yao makubwa ni kuweza kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara jambo wanaloamini kwamba litatimia.
Kwenye mzunguko wa kwanza Yanga ilianza kwa kasi nzuri na ilicheza jumla ya mechi 19 bila kupoteza ila ilipocheza mechi tano ilibadili benchi la ufundi kwa kumfuta kazi Zlatko Krmpotic.
Mrithi wa mikoba yake, Cedric Kaze yeye aliongoza Kwenye mechi 18, alishinda 10, sare 7 na kichapo moja akachimbishwa Machi 7 kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni mwendo mbovu wa timu.
Ikiwa ipo nafasi ya Kwanza imekuwa ikipata presha kubwa kutoka kwa watani zao wa jadi Simba ambao ni Mabingwa watetezi wapo nafasi ya pili na pointi zao ni 46 huku vinara wakiwa na pointi 50.
Mshindo Msola Mwenyekiti wa Yanga amesema:"Malengo ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara yapo palepale,".
Credit: SALEH JEMBE
Please subscribe to get all sports news instantly
COMMENTS