Tanzania Yatoa Muelekeo Wake Katika Awamu Ya Pili Ya Uongozi Wa Rais Magufuli
HomeHabari

Tanzania Yatoa Muelekeo Wake Katika Awamu Ya Pili Ya Uongozi Wa Rais Magufuli

Serikali ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesema katika kipindi cha muhula wa pili wa miaka mitano ya Rais Dkt. John Pombe Joseph Mag...

Polisi Watakiwa Kuongeza Kasi Ya Ukusanyaji Mapato
Serikali Yazihakikishia Kampuni Za Uswisi Mazingira Salama Ya Biashara, Uwekezaji
Waziri Simbachawene Azindua Mfumo Udhibiti Ajali Barabarani, Jijini Arusha


Serikali ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesema katika kipindi cha muhula wa pili wa miaka mitano ya Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli itajikita zaidi katika diplomasia ya uchumi, kuimarisha sekta binafsi, kukuza biashara pamoja na mahusiano na Mataifa mengine duniani.

Msimamo wa Tanzania umetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi Jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano wake na Mabalozi wanaoziwakilisha Nchi zao hapa Tanzania pamoja na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa na kuongeza kuwa ni dhamira ya Tanzania kuhakikisha kuwa ina uwezo wa kukuza biashara na kuuza bidhaa katika nchi mbalimbali duniani.

“Katika mwaka huu unaoanza sasa na miaka ijayo katika mhula wa pili awamu ya tano ni wakati muafaka wa Tanzania kuimarisha diplomasia ya uchumi na uhusiano mwema baina yake na nchi mbalimbali kwa kuwakaribisha wawekezaji kutoka nchi hizo katika maeneno ya uzalishaji, viwanda na kuongeza biashara kwa manufaa ya mataifa yote,” Amesema Prof. Kabudi

Pamoja na mambo mengine, Prof. Kabudi amewaambia Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa hapa Nchini kuwa hali ya kisiasa na amani Zanzibar na Tanzania kwa ujumla imeimarika kuliko wakati wowote hususani mara baada ya uchaguzi mkuu uliomalizika Octoba, 2020 na kwamba uwepo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar unachochea kuongezeka kwa uwekezaji na ufanyaji wa biashara kwa lengo la kukuza uchumi.

Kwa upande wake Kiongozi wa Mabalozi Dkt. Ahmada El Badasui ambaye pia ni Balozi wa Comoro hapa nchini ameshukuru kwa uwepo wa mkutano huo ambao unawapa fursa mabalozi kufahamu masuala mbalimbali yanayoendelea hapa nchini.

“Nakupongeza Mhe. Waziri na uongozi wa Wizara kwa kuandaa mkutano huu ambao unatupa fursa sisi mabalozi kujadili na kujua mambo mbalimbali yanayoendelea hapa nchini, mikutano kama hii ni muhimu sana kwetu kwani inatusaidia na kutuwezesha kuboresha mahusiano yetu ya kidiplomasia,” Amesema Dkt. El Badasui

Kwa upande wake Balozi wa Umoja wa Ulaya Mhe. Manfredo Fanti ameipongeza Tanzania kwa kuingia uchumi wa kati na kwamba Umoja wa Ulaya uko tayari kutoa ushirikiano wa kutosha ili kuhakikisha Uchumi wa Tanzania unaendelea kukua na kuimarika.

Mkutano huo wa Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa umehudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe William Tate Ole Nasha, Katibu Mkuu Balozi, Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge na Wakurugenzi na Wakuu wa Idara na vitengo vya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Tanzania Yatoa Muelekeo Wake Katika Awamu Ya Pili Ya Uongozi Wa Rais Magufuli
Tanzania Yatoa Muelekeo Wake Katika Awamu Ya Pili Ya Uongozi Wa Rais Magufuli
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEish2t0UBQhp8MKL89BaLvGSF7M4ZzZA9zg6G0l4BBMhs5-W6_YxCe6GpN_NDeLTOpsjmgXEicUJITWxw-TyZzAlZS7OZpbmy4zbUX8ngDXKvSbVKBK0HUg51QgfG9RetXmNkNGX-YSGxW5/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEish2t0UBQhp8MKL89BaLvGSF7M4ZzZA9zg6G0l4BBMhs5-W6_YxCe6GpN_NDeLTOpsjmgXEicUJITWxw-TyZzAlZS7OZpbmy4zbUX8ngDXKvSbVKBK0HUg51QgfG9RetXmNkNGX-YSGxW5/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/tanzania-yatoa-muelekeo-wake-katika.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/tanzania-yatoa-muelekeo-wake-katika.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy