MCHEZO MZIMA WA YANGA KUTINGA 16 BORA ULIKUWA NAMNA HII
HomeMichezo

MCHEZO MZIMA WA YANGA KUTINGA 16 BORA ULIKUWA NAMNA HII

  FISTON Abdol Razack nyota mpya wa Yanga jana alifunga bao lake la kwanza ndani ya timu hiyo ambalo liliipa nafasi ya kusonga mbele hatua...

VIDEO: SAIDA KARORI: NILILA CHUMBA CHA BUKU TANO
BUKAYO, RASHFORD NA SANCHO WAKUTANA NA UBAGUZI WA RANGI
SIMBA QUEENS WAPANIA KIMATAIFA

 FISTON Abdol Razack nyota mpya wa Yanga jana alifunga bao lake la kwanza ndani ya timu hiyo ambalo liliipa nafasi ya kusonga mbele hatua ya 16 bora kwenye mashindano ya Kombe la Shirikisho.

Bao hilo alipachika kwa penalti dakika ya 40 baada ya mpira kumfuata kwenye mkono nyota wa Ken Gold wakati Yanga walipokuwa wakifanya mashambulizi.

Jitihada za Yanga kuongeza bao la pili ndani ya dakika tano zilikwama baada ya Adam John, kipa wa Ken Gold kuwa kisiki kwa nyota wengi wa Yanga ambao walikuwa wakifanya majaribio kusaka ushindi.

Ni Fei Toto dakika 16 alipaisha mpira akiwa nje kidogo ya lango huku Fiston naye akionekana kukosa utulivu ndani ya eneo la 18.

Kipindi cha pili Ken Gold waliongeza juhudi kuweza kutafuta ushindi ila walikwama kumfunga Faroukh Shikalo ambaye aliweza kuokoa hatari.

Nyota Carlos Carlinhos alitumia dakika 14 ndani ya Uwanja wa Uhuru ambapo alifanya jaribio moja na kupiga kona mbili kabla ya kuonyeshwa kadi nyekundu ya moja kwa moja kutokana na kitendo chake cha kumpiga ngumi mchezaji wa Ken Gold.

Hivyo atakosa mechi tatu zijazo ndani ya kikosi cha Yanga ambacho mchezo wake ujao ni wa ligi dhidi ya Coastal Union. 

Kocha Mkuu wa Yanga, Cedric Kaze amesema kuwa ushindi ambao wameupata ni mwendelezo wa safari yao kuelekea yalipo malengo ya kutwaa taji la Kombe la Shirikisho.

Beki Boniface Mwanjonde wa Ken Gold ambaye alikutana na kitasa cha Carlinhos amesema kuwa jitihada zao zilikwama licha ya kupambana kusaka ushindi.

Ushindi huo unaifanya Yanga kusubiri mshindi wa mchezo wa leo kati ya Sahare All Stars ama Tanzania Prisons ili wacheze naye hatua ya 16 bora.



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: MCHEZO MZIMA WA YANGA KUTINGA 16 BORA ULIKUWA NAMNA HII
MCHEZO MZIMA WA YANGA KUTINGA 16 BORA ULIKUWA NAMNA HII
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgOQvB0CMJQplKj7Lz21o0WlZffQkUwz-XFxqiOXvcnHHyOJseTdiJxXL3TwT5uXuIsiB1ZkJJD1ALricCYZZ0Pox4fVHjRD1abzjb2xLhH43BOALDYsJbhzl6TMHF9HZbE72pda-ZTUDu7/w640-h602/Fiston+goal.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgOQvB0CMJQplKj7Lz21o0WlZffQkUwz-XFxqiOXvcnHHyOJseTdiJxXL3TwT5uXuIsiB1ZkJJD1ALricCYZZ0Pox4fVHjRD1abzjb2xLhH43BOALDYsJbhzl6TMHF9HZbE72pda-ZTUDu7/s72-w640-c-h602/Fiston+goal.JPG
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/mchezo-mzima-wa-yanga-kutinga-16-bora.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/mchezo-mzima-wa-yanga-kutinga-16-bora.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy