Majaliwa: Watendaji Zitafutieni Ufumbuzi Kero Za Wananchi
HomeHabari

Majaliwa: Watendaji Zitafutieni Ufumbuzi Kero Za Wananchi

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amewataka viongozi na watendaji wote wa Serikali wahakikishe wanawafikia wananchi kwenye maeneo yao, kusikil...

Kiongozi wa upinzani auawa Burundi
Urais 2015: Mwanamke wa kwanza CCM ajitokeza kutangaza nia
Lowassa Na Wenzake Sasa Wako Huru....Adhabu Yao Ilikwisha Jana......Taarifa Kamili iko Hapa


WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amewataka viongozi na watendaji wote wa Serikali wahakikishe wanawafikia wananchi kwenye maeneo yao, kusikiliza kero zao na kuzitafutia ufumbuzi.

“Tunapaswa kuwajibika kwao badala ya kusubiri ziara za viongozi wakuu wa Kitaifa. Natumia fursa hii kuwaambia viongozi na watendaji wote wa Serikali kuwa tutapima utendaji wenu kwa namna mnavyotatua kero za wananchi kwenye maeneo yenu. ”

Ameyasema hayo jana (Ijumaa, Februari 5, 2021) wakati akihitimisha hoja ya kujadili hotuba ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli aliyoitoa wakati wa ufunguzi wa bunge la 12 Novemba 13, 2020. Amesema watendaji hao wana wajibu kwa wananchi kutokana na dhamana waliyowapatia.

Hivyo, Waziri Mkuu ametoa wito kwa kila mtendaji Serikalini ahakikishe anatimiza wajibu wake kikamilifu na Serikali kwa upande wake itahakikisha inachukua hatua dhidi ya wote watakaokiuka sheria, kanuni na taratibu za kazi na kamwe haitomvumilia mtumishi mzembe na mwenye kufanya kazi kwa mazoea.

Amesema nchi imekuwa ikifanya juhudi kubwa katika kuandaa mipango na bajeti kwa ajili ya utekelezaji wa vipaumbele mbalimbali vya Serikali vyenye lengo la kuwaletea maendeleo wananchi, hata hivyo, awali kulikuwa na changamoto ya baadhi ya viongozi na watendaji kutowajibika ipasavyo kwa wananchi.

Waziri Mkuu amesema katika kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali ya Awamu ya Tano ilijikita katika kuhakikisha inarejesha nidhamu katika Utumishi wa Umma kwa kuweka mkazo katika misingi ya uadilifu, uwajibikaji, kutoa huduma kwa wakati na kuchukua hatua za haraka dhidi ya watumishi wote wanaokwenda kinyume na misingi ya utendaji kazi Serikalini.

Kadhalika, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwahakikishia wabunge kwamba maoni na hoja zao zitazingatiwa wakati wote wa utekelezaji wa vipaumbele vya Serikali.

Amesema kuhusu miradi inayoendelea kutekelezwa nchini katika sekta za uzalishaji mali ikiwemo kilimo, mifugo, maliasili, madini na sekta za huduma ya jamii, kama vile elimu na afya nayo itakamilishwa kama ilivyokusudiwa.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Majaliwa: Watendaji Zitafutieni Ufumbuzi Kero Za Wananchi
Majaliwa: Watendaji Zitafutieni Ufumbuzi Kero Za Wananchi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhvDzIP45Y4O1K8m2oOrdZYlqTQp4q7YiyXiomb4ttC19IgPGe1tmkP9lP8KUnEuwZQ9pi47g93kfcsb9LCniJsigcqh_BJYRUHJ2NzoGSdudazvsKHIPxbD0FxvNGqfoVJCUYwrMzDHt_s/s16000/1.jpeg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhvDzIP45Y4O1K8m2oOrdZYlqTQp4q7YiyXiomb4ttC19IgPGe1tmkP9lP8KUnEuwZQ9pi47g93kfcsb9LCniJsigcqh_BJYRUHJ2NzoGSdudazvsKHIPxbD0FxvNGqfoVJCUYwrMzDHt_s/s72-c/1.jpeg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/majaliwa-watendaji-zitafutieni-ufumbuzi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/majaliwa-watendaji-zitafutieni-ufumbuzi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy