YANGA YABANWA KILA KONA, YATOKA 0-0 NA RUVU SHOOTINGS
FT: YANGA 0 : 0 RUVU SHOOTINGS
HomeHabariKitaifa

YANGA YABANWA KILA KONA, YATOKA 0-0 NA RUVU SHOOTINGS

FT: YANGA 0 : 0 RUVU SHOOTINGS Dakika za lala salama Yanga wanatafuta njia ya kufunga goli, lakini mabeki wa Shootings wamesimama...



Dakika za lala salama Yanga wanatafuta njia ya kufunga goli, lakini mabeki wa Shootings wamesimama imara
Dakika +4′ za nyongeza
Dakika 90 zimeshamalizika hakuna timu iliyoona lango la mwenzake
Dakika ya 89′ kunatokea Sintofahamu baina ya kipa wa Yanga na mchezaji wa Shootings baada ya Yondani kumfanyia madhambi mchezaji pinzani
Dakika ya 89′ kunatokea Sintofahamu baina ya kipa wa Yanga na mchezaji wa Shootings baada ya Yondani kumfanyia madhambi mchezaji pinzani
Dakika ya 83′ Salvatory Ntebe  anaoneshwa kadi nyekundu
Dakika ya 81′ Rajab Zahiri ameiokoa Yanga katika hatari baada ya mshambulizi wa Shooting, Abdulrahman Mussa kubaki yeye na kipa na mpira kuwa kona ambayo haikuzaa matunda
Dakika ya 80′ si Yanga wala Shootings iliyoona lango la mwenzake
Dakika ya 78′ Niyonzima anapiga mpira wa adhabu ndogo kutoka winga ya kulia lakini mabeki wa Shootings wanaokoa

Dakika ya 75′ milango ya timu zote bado ni migumu na Yanga wanashindwa kutumia kona waliyopata baada ya mabeki wa Shootings kuokoa
Dakika ya 73′ Yanga wanapata kona, lakini kipa Abdallah Rashind ameanguka chini na anatibiwa
Dakika ya 71′ Hussein Javu anaingia kuchukua nafasi ya Coutinho
Dakika ya 68′ Jerome Lambele anaingia kuchukua nafasi ya Mwita Kemalonge
Dakika ya 68′ Mpira umesimama baada ya mchezaji wa Shootings kufanyiwa madhambi
Dakika ya 65′ Msuva anakwenda benchi nafasi yake inachukuliwa na Daniel ‘Danny’ Davis Mrwanda

TAIFA: Dakika ya 61 hakuna timu iliyopata goli kati ya Yanga na Ruvu Shootings..
………………………………………………………………
NDANDA 0 : 2 SIMBA SC
………………..kutoka Mtwara, Elius Maguri anaifungia Simba bao la pili katika dakika ya 52 akipokea pasi ya Danny Sserunkuma.
………………………………………………………………….
Dakika ya 55′ Yahya Tumbo anakwenda benchi kwa upande wa Ruvu Shootings nafasi yake inachukuliwa na Baraka Mtuwi
Dakika ya 51′ bado milango ni migumu
Dakika ya 47′ hakuna timu iliyoona lango baina ya Yanga na Ruvu Shootings
UWANJA WA TAIFA: YANGA 0 : 0 RUVU SHOOTINGS
………………………………………..
HT: STAND UNITED 0 : 1 AZAM FC
Dakika ya 43, Frank Domayo ameifungia goli la kuongoza Azam fc dhidi ya wenyeji Stand United
KUTOKA NAGWANDA SIJAONA MTWARA…Mpira ni mapumziko Simba wakiwa mbele kwa goli moja lililofungwa na Danny Sserunkuma katika dakika ya 32 kipindi cha kwanza akimalizia mpira wa kona uliopigwa na Elius Maguri
…………………………………….
HT: YANGA 0 : 0 RUVU SHOOTINGS
Dakika ya sita ya nyongeza badala ya tano Yanga wamepata kona mbili mfululizo, lakini hazijazaa matunda
Dakika ya mwisho ya nyongeza kumetokea piga nikupige eneo la Shootings, lakini mabeki wanaokoa.

Dakika 45 zimekamilika na mwamuzi anongeza dakika tano za nyongeza
Dakika ya 44 Shootings wamepoteza nafasi nzuri ya kufunga
Dakika ya 40 Msuva anakosa nafasi nyingine baada ya kuwekewa mpira na Edward Charles. Mpira huo ulitokana na mpira wa kona kufuatia shuti la Tambwe kuokolewa na kipa Rashid

Dakika ya 39′ Msuva anakosa bao akiwa yeye na kipa
Dakika ya 36′ Yanga wanapata kona ambayo haizai matunda
Dakika ya 33′ Coutinho anapiga mpira wa adhabu ndogo unaowababatiza mabeki wa Shootings na kumchanganya kipa Rashid, lakini anajitahidi kuokoa
Dakika ya 25′ Coutinho amekosa bao baada ya kichwa chake kutoka nje ya lango akiunganisha krosi ya Niyonzima kutoka winga ya kulia
Dakika ya 24′ hakuna timu iliyoona lango la mwenzake
Dakika ya 19′ Tambwe amefunga goli kwa mkono mwamuzi anakataa na kumuonesha kadi ya njano

Dakika ya 18′ Saimon Msuva anaoneshwa kadi ya njano
Dakika ya 17 mpira umesimama baada ya Msuva kumfanyiwa madhambi mchezaji wa Shootings ambaye yuko chini
Dakika ya 12′ Andrey Coutinho amepiga mpira wa adhabu ndogo ndani ya eneo la 18, lakini mlinda mlango Rashid Abdallah ameokoa
Dakika ya 6′ kipindi cha kwanza Yanga wanagongeana pasi eneo lao, lakini wanashindwa kuvuka kirahisi eneo la Shootings kutokana na ulinzi waliowekewa
Dakika ya 4′ Yanga wameanza kwa kasi wakifika mara kadhaa langoni kwa Shootings lakini mipango haijawa sawa

Yanga wamepata kona sekunde kadhaa lakini haijazaa matunda
Mpira umeshaanza hapa uwanja wa Taifa Yanga wakiwa wa kwanza kugusa mpira
Wachezaji wanasalimiana tayari kwa kuanza kipute
Wachezaji wa timu zote wameingia uwanjani tayari kwa kukaguliwa na waamuzi

Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: YANGA YABANWA KILA KONA, YATOKA 0-0 NA RUVU SHOOTINGS
YANGA YABANWA KILA KONA, YATOKA 0-0 NA RUVU SHOOTINGS
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/MMGM0029-1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/yanga-yabanwa-kila-kona-yatoka-0-0-na.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/yanga-yabanwa-kila-kona-yatoka-0-0-na.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy