WAGONGA nyundo wa Mbeya, Mbeya City fc wameanza kurejesha makali yao baada ya kuitandika bao 1-0 Kagera Sugar katika mechi ya ligi k...
WAGONGA nyundo wa Mbeya, Mbeya
City fc wameanza kurejesha makali yao baada ya kuitandika bao 1-0 Kagera
Sugar katika mechi ya ligi kuu soka Tanzania bara iliyomalizika jioni
hii uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.
Bao hilo pekee limefungwa dakika ya 80 na Peter Mapunda.
Kikosi hicho cha Juma Mwambusi kilishangiliwa na zaidi ya mashabiki 200 waliosafiri kutoka Mbeya kuipa sapoti timu hiyo.
Ushindi wa huu ni wapili
mfululizo kwani desemba 28 mwaka jana waliibuka na ushindi wa bao 1-0
dhidi ya Ndanda fc katika mechi ya raundi ya nane ya ligi kuu kwenye
uwanja wa Sokoine Mbeya.
COMMENTS