AFCON:Kundi B limemenyana vikali
HomeMichezoKimataifa

AFCON:Kundi B limemenyana vikali

Kindumbwendumbwe cha michuano ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kinaendelea nchini Equatorial Guinea ambapo mzunguko wa pili ...

Boko Haram Appears to Be Using Abducted Girls as Suicide Bombers: Experts
Mashambulizi ya Boko Haram ni ya ukatili dhidi ya binadamu
Man U:wamtimua Torben Aakjaer

Kindumbwendumbwe cha michuano ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kinaendelea nchini Equatorial Guinea ambapo mzunguko wa pili uliendelea jana kwa timu za kundi B kumenyana. Katika mchezo wa awali wa kundi hilo Tunisia iliinyuka Zambia mabao 2-1. Katika mchezo huo Zambia ndio waliokuwa wa kwanza kuziona nyavu za Tunisia katika dakika ya 59 likifungwa na Mayuka. Tunisia iliamka na kusawazisha katika dakika ya 70 kupitia kwa Akaichi na Chikhaoui akamaliza kazi katika dakika ya 88 kwa kukwamisha mpira langoni mwa Zambia. Kukosa umakini katika safu ya ushambuliaji na ulinzi kuliikosesha Zambia ushindi katika mchezo huo.

Katika mchezo wa pili wa kundi B, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na Cape Verde zilitoka sare ya kutofungana huku kila timu ikishindwa kutumia nafasi ilizotengeneza kupata magoli. Kwa matokeo hayo Tunisia sasa inaongoza ikiwa na pointi nne, ikifuatiwa na timu za Cape Verde na DR Congo zenye pointi mbili kila moja na mkiani ni Zambia yenye pointi moja. Kabla ya michezo yao ya jana timu hizo zilikuwa na pointi moja kila moja.

Mzunguko wa pili utaendelea kwa timu za kundi C kupambana. Ghana itaumana na Algeria, ambapo Afrika Kusini itahenyeshana na Senegal katika mchezo wa pili wa kundi hilo. Katika mechi za kwanza kwa timu hizo, Algeria iliizamisha Afrika Kusini kwa mabao 3-1, huku Senegal ikiinyamazisha Ghana kwa kuichapa 2-1.
 
Nazo timu za kundi D za Ivory Coast, Mali, Cameroon na Guinea zitaonyeshana kazi kazi kesho, Jumamosi. Ivory Coast itaumana na Mali, huku Cameroon ikipambana vikali na Guinea. Timu za kundi hili zina pointi moja moja kabla ya mpambano wao wa mzunguko wa pili
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: AFCON:Kundi B limemenyana vikali
AFCON:Kundi B limemenyana vikali
http://ichef.bbci.co.uk/news/ws/660/amz/worldservice/live/assets/images/2015/01/23/150123000459_tunisia_512x288_bbc_nocredit.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/afconkundi-b-limemenyana-vikali.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/afconkundi-b-limemenyana-vikali.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy