Uvutaji bangi,uporaji,wizi,wakera baraza la Madiwani Manispaa ya Geita
HomeHabariTop Stories

Uvutaji bangi,uporaji,wizi,wakera baraza la Madiwani Manispaa ya Geita

Baraza la Madiwani katika Manispaa ya Geita Mkoani Geita limesikitishwa na Baadhi ya Vitendo vya Uvunjifu wa amani ambavyo vimekuwa vikifany...

Baraza la Madiwani katika Manispaa ya Geita Mkoani Geita limesikitishwa na Baadhi ya Vitendo vya Uvunjifu wa amani ambavyo vimekuwa vikifanywa na Baadhi ya Vijana wilayani humo huku wakiviomba vyombo vya Usalama kuingilia kati Uharifu unaofanywa na Vijana hao.

Hayo yameelezwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wakati wakijadili taarifa ya robo ya Pili ya Mwaka 2024/ 2025 ambapo Baadhi ya Madiwani akiwemo Diwani wa kata ya Bombambili Leonard Bugomola na Zaituni Fundikira Diwani wa Viti Maalumu kata ya Kalangalala wamepaza sauti ya kuwepo kwa vitendo vya wizi , uvutaji Bangi pamoja na wananchi kuporwa Mali zao.

” Vile vikundi vya waharifu ambao wamekwenda kwenye eneo la uwekezaji Bombambili wanaovuta bangi sikanka na vitu vingine ambavyo vinapelekea watoto badala ya kuingia madarasani wanakwenda kukaa na tumesha kuwakurupusha zaidi ya Mara mbili mara tatu sasa ndio maana hii changamoto nimeileta ili tuweze kupatiwa ufumbuzi , ” Diwani kata ya Bombambili , Leonard Bugomola.

Katika hatua nyingine Diwani wa Viti Maalumu kutokea kata ya Kalangalala Bi. Zaituni Fundikira amesema changamoto iliyopo katika Mitaa ya Kalangalala ukiwemo mtaa wa mission ni uwepo wa watoto wanaoishi katika Mazingira magumu ambao wamekuwa kichocheo cha Matendo ya uharifu ikiwemo kuvunja nyumba na kuiba vitu mbalimbali.

” Mh Mwenyekiti hawa watoto wa mtaani tumejitahidi kuwafukuza na tumejitahidi kuwafanyia utaratibu wa kuwarudisha ndio maana wanazaa athari mbaya kwa watoto wetu wengine ambao ni watoto wazuri Mh Mwenyekiti hawa watoto wanatupa athari kubwa kwenye majumba yetu kwa sababu mtaa wetu wa mission wameenda kuiba na wanabomoa wanadumbukiza wale watoto wanaiba lakini walinzi walijitahidi kuwakamata , ” Diwani wa viti maalumu kata ya Kalangalala , Zaituni Fundikira.

Janeth Mobe ni Mwakilishi wa Mkuu wa wilaya ya Geita katika Baraza hilo amesema tayari Ofisi ya Mkuu wa wilaya kwa kushirikiana na Vyombo vya Usalama wameanza kufanya Doria ya kuwasaka watu hao ambao wamekuwa wakifanya virendo hivyo na kupelekea kuvunja sheria za nchi.

“Ni kweli kuna shida kunaanza kuteteleka suala la usalama pale Bugulula kuja Geita ama kutoka kamwanga kuja Geita changamoto iko kubwa Bodaboda pale tujipange jambo hili sasa linatia shaka ko palikuwa na utulivu lakini sasa naona kam vile wanaona sijui serikali imejisahau wameanza vibaka vibaka pale ikifika jioni wanavizia watu na samaki wanavizia Bodaboda nadhani kama ulivyosema das niwapongeze kwa kuliona hilo , ” Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Geita, Barnabas Mapande.

The post Uvutaji bangi,uporaji,wizi,wakera baraza la Madiwani Manispaa ya Geita first appeared on Millard Ayo.



from Millard Ayo https://ift.tt/CWif5ba
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Uvutaji bangi,uporaji,wizi,wakera baraza la Madiwani Manispaa ya Geita
Uvutaji bangi,uporaji,wizi,wakera baraza la Madiwani Manispaa ya Geita
https://millardayo.com/wp-content/uploads/2025/02/IMG-20250208-WA0054-633x950.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2025/02/uvutaji-bangiuporajiwiziwakera-baraza.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2025/02/uvutaji-bangiuporajiwiziwakera-baraza.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy