NCCR-Mageuzi Yamsimamisha Mbatia
HomeHabari

NCCR-Mageuzi Yamsimamisha Mbatia

Halmashauri kuu  ya Chama cha NCCR-Mageuzi, imemsimamisha Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, James Mbatia na Makamu Mwenyekiti wake Bara, A...

Majaliwa: Viongozi Wa Dini Wekezeni Katika Malezi Ya Vijana,ashuhudia Kusimikwa Kwa Askofu, Lushoto Tanga
Uadilifu Kuwezesha Ukuaji Wa Uchumi Wa Blue
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo May 10

Halmashauri kuu  ya Chama cha NCCR-Mageuzi, imemsimamisha Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, James Mbatia na Makamu Mwenyekiti wake Bara, Angelina Mtaigwa, kwa tuhuma mbalimbali ikiwemo ukiukwaji wa maadili.

Uamuzi huo umetangazwa Jumamosi, tarehe 21 Mei 2022 na Mwenyekiti wa kikao cha halmashauri hiyo kilichoketi jijini Dar es Salaam, Joseph Selasini.

Akisoma maazimio ya halmashauri hiyo, Selasini amedai Mbatia amesimamishwa katika wadhifa huo kutokana na kutokuwa na mahusiano mazuri na makatibu wake.

Hivi karibuni, Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Martha Chiomba, alidai kulazimishwa kujiuzulu na Mbatia, tuhuma ambazo mwanasiasa huyo alizikanusha.

“Tulielezwa jinsi ambavyo mwenyekiti alimtaka katibu mkuu ajiuzulu na ikumbukwe hana zaidi ya mwaka ndani ya chama na katika mjadala tumekubaliana alikuwa anabadilisha makatibu wakuu jinsi anavyotaka. Sasa huyu ni katibu wa sita tangu alivyokuwa mwenyekiti,” amedai Selasini.

Selasini ametaja sababu nyingine za Mbatia kusimamishwa, akidai anatuhumiwa kwa kukisabisha chama hicho kisishiriki mikutano mbalimbali iliyotitishwa kwa ajili ya kujadili masuala ya demokrasia ya vyama vingi, ikiwemo ulioitishwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD).

Amedai, awali chama hicho kilikataa kushiriki vikao hivyo hadi Serikali itakapokuwa na nia njema dhidi ya viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani, ikiwemo kuachwa huru kwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, aliyekuwa rumande katika Gereza la Ukonga, kwa tuhuma za ugaidi.

Selasini amedai, baada ya Mbowe kuachwa huru Machi 2022, NCCR-Mageuzi haikuwa na kikwazo cha kushiriki vikao hivyo lakini Mbatia aliitisha kikao cha kamati cha dharura kubatilisha uamuzi huo.

Selasini amedai maazimio ya halmashauri hiyo kumsimamisha Mbatia ni halali, kwani akidi ya wajumbe wake ilikidhi matakwa ya kisheria ambapo waliohudhuria ni 52 kati ya wajumbe 82.

“Kabla ya mjadala haujaanza ulizuka mjadala wa Mwenyekiti wa chama kutokuwepo katika mkutano huu na taarifa ilitolewa kwamba anazo taarifa za mkutano akishiriki kuuitisha na baada ya kusubiri kwa muda bila kujulikana na wajumbe wako tayari ukumbi tukaona mkutano uendelee,” amesema Selasini.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: NCCR-Mageuzi Yamsimamisha Mbatia
NCCR-Mageuzi Yamsimamisha Mbatia
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjsN3GmW1UPxYFCsgzO7c1IQrSrl3HPLZgMCm3_xaNS8bFneYDUM8wSRfuMkKCy3nf-DWds972v1121ZnIiE_pTVBb-ZYqDoozeuOAj9NEprleSxUr59DPKwcIJz0im7U1J5krPwRUTiRrNSjDx7XljeO4xhUuC3-ImdDAXGC5kJ13_l0MOZHtULSNAyA/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjsN3GmW1UPxYFCsgzO7c1IQrSrl3HPLZgMCm3_xaNS8bFneYDUM8wSRfuMkKCy3nf-DWds972v1121ZnIiE_pTVBb-ZYqDoozeuOAj9NEprleSxUr59DPKwcIJz0im7U1J5krPwRUTiRrNSjDx7XljeO4xhUuC3-ImdDAXGC5kJ13_l0MOZHtULSNAyA/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/05/nccr-mageuzi-yamsimamisha-mbatia.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/05/nccr-mageuzi-yamsimamisha-mbatia.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy