Changamoto Ya Upungufu Wa Dawa Yaenda Kuwa Historia
HomeHabari

Changamoto Ya Upungufu Wa Dawa Yaenda Kuwa Historia

Na. WAF – Kigoma Changamoto ya upungufu wa dawa inaenda kuwa historia nchini baada ya Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi kupig...


Na. WAF – Kigoma
Changamoto ya upungufu wa dawa inaenda kuwa historia nchini baada ya Katibu Mkuu Wizara ya Afya Prof. Abel Makubi kupiga marufu utolewaji wa fomu namba 2C kuanzia July 1, 2022 ambayo ilikua ikitoa mwanya kwa baadhi watoa huduma kufanya udanganyifu.

Marufuku hiyo ameitoa kwenye kikao na watumishi wa Afya mkoani Kigoma kilichohudhuriwa pia na Mganga mkuu wa Mkoa Kigoma Dkt. Jeska Leba Baada ya kufanya ziara fupi katika hospitali hiyo.

Prof. Makubi amesema kuwa kuna baadhi ya watoa huduma wamekuwa wakitumia fomu hiyo vibaya kwa kuwaandikia dawa wagonjwa kwenda kununua nje ya kituo cha kutolea huduma ya Afya cha Serikali.

“Hii imekua ni uchochoro kwa wapigaji lakini pia ni usumbufu kwa mgonjwa kwenda kununua dawa nje, hivyo dawa zinatakiwa zijazwe kwenye hospitali za Serikali na kuacha kuwanufaisha wengine.” Amesema Prof. Makubi

Aidha, katika kikao hicho Prof. Makubi amebainisha mambo kadhaa muhimu ya kuzingatia kwa watumishi hao wa Afya ikiwemo kuhakikisha sekta ya Afya inafanya vizuri katika uongozi na uwajibikaji kwenye kutoa huduma nzuri.

Pia, kuwa na lugha nzuri wakati wa kutoa huduma, kuwajibika kazini, kuhakikisha ubora wa huduma za tiba na kinga, ukaguzi wa mara kwa mara, kuendelea kutoa chanjo pamoja na elimu za chanjo mbalimbali na kujali Afya ya mama na mtoto.

Prof. Makubi katika ziara hiyo ametembelea miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ya ujenzi na ukarabati wa majengo na kubaini baadhi ya changamoto ikiwemo ya mradi wa Jengo la wagonjwa wa nje (OPD) linalosuasua na kutoa maagizo hadi ifikapo Juni 30, 2022 liwe limekamilika.

“Muache mazoea kwenye kazi, mmepewa kazi na hela zote mmelipwa nataka mkamilishe mradi wa jengo hili kabla ya Juni 30, 2022 fanyeni kazi usiku na mchana na ikiwezekana ongezeni vibarua.” Alisisitiza Prof. Makubi

Hata hivyo, Prof. Makubi amewasifu viongozi na watendaji wanaosimamia mradi wa ujenzi wa jengo la dharula (EMD) ambapo ujenzi wa jengo hilo unaendelea vizuri na umegharimu jumla ya shilingi Bilioni 1.3.

“Miradi yote hii mjitahidi muimalize kwa wakati. Mfanye kazi usiku na mchana, ongezeni vibarua kazi ikamilike bila kuharibu ubora kwa kuwa wananchi wanataka huduma bora ya yenye mazingira rafiki kwao.” Amesema Prof. Makubi

Miongoni mwa miradi ya majengo katika hospitali hiyo ya Rufaa Mkoa wa Kigoma ni pamoja na jengo la upasuaji, jengo la kutakasishia vifaa vya kutolea huduma (CSSD), jengo la Monchwari, jengo la dharula (EMD), jengo la wagonjwa wa nje (OPD) pamoja na jengo la tiba mtandao ambalo limekamilika kwa asilimia 100.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Changamoto Ya Upungufu Wa Dawa Yaenda Kuwa Historia
Changamoto Ya Upungufu Wa Dawa Yaenda Kuwa Historia
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhnKJFp24yUJTvWIieZBUlkw9FSMN7b0EgSnH7oXamy3FDJy4kbyuAUWaCVV8-28d2WogPc-pXOi21f2dF0p_Eep6A3wqrYmwvswdhBXQNEUk7mH0DOFIIf6Aah9D0qeICYF5IpGkKRvfqcCTcskoddWiSE_Bf0iLCuKqFSkmg2Qbs6PXGnz0bp-aa24A/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhnKJFp24yUJTvWIieZBUlkw9FSMN7b0EgSnH7oXamy3FDJy4kbyuAUWaCVV8-28d2WogPc-pXOi21f2dF0p_Eep6A3wqrYmwvswdhBXQNEUk7mH0DOFIIf6Aah9D0qeICYF5IpGkKRvfqcCTcskoddWiSE_Bf0iLCuKqFSkmg2Qbs6PXGnz0bp-aa24A/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/05/changamoto-ya-upungufu-wa-dawa-yaenda.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/05/changamoto-ya-upungufu-wa-dawa-yaenda.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy