Dkt. Nchemba: Serikali Kuwekeza Zaidi Kwenye Sekta Za Uzalishaji
HomeHabari

Dkt. Nchemba: Serikali Kuwekeza Zaidi Kwenye Sekta Za Uzalishaji

Na Benny Mwaipaja, Dodoma   WAZIRI wa Fedha na Mipango, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, ameliambia Shirika la Maendeleo la Umoj...


Na Benny Mwaipaja, Dodoma
 
WAZIRI wa Fedha na Mipango, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, ameliambia Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) kwamba Serikali imejipanga kikamilifu kuhakikisha kuwa sekta muhimu za uzalishaji zinaongezewa fedha ili kuongeza tija katika sekta hizo.
 
Dkt. Nchemba aliyasema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe wa Shirika hilo ukiongozwa na Mwakilishi wake Mkazi Bi. Christine Musisi, Jijini Dodoma.
 
“Katika Bajeti ya mwaka 2022/2023, na zijazo, tutawekeza fedha nyingi kwenye maeneo ya uzalishaji ikiwemo kilimo kwa kuongeza huduma za umwagiliaji na uzalishaji wa mbegu bora, uhifadhi wa mazao, mifugo bora, uvuvi na kuboresha mazingira ya biashara kwa wamachinga” alieleza Dkt. Nchemba
 
Alisema kuwa sekta hizo ni kipaumbele cha Serikali ya Awamu ya Sita, inayoongozwa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na inakwenda sambamba na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya mwaka 2025 na Utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano.
 
Dkt. Nchemba, alilipongeza Shirika hilo la Maendeleo la Umoja wa Mataifa – UNDP kwa kuchangia maendeleo ya nchi katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na kijamii na kuliomba Shirika hilo kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali za kuwaletea wananchi maendeleo.
 
Naye Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Amina Khamis Shaaban, alisema kuwa Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano unakadiriwa kugharimu shilingi trilioni 114.8 ambapo kati ya fedha hizo, shilingi trilioni 40.6 zinatakiwa zitoke Sekta Binafsi na kuliomba UNDP, kusaidia upatikanaji wa fedha hizo kwa kushirikiana na washirika wake mbalimbali.
 
Kwa upande wake Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa mataifa-UNDP, Bi. Christine Musisi, ameihakikishia Tanzania kwamba Shirika lake litaendelea kushirikiana nayo kuchangia maendeleo ya kiuchumi na kijamii kupitia miradi mbalimbali iliyowekeza fedha nchini ikiwemo kilimo, uchumi wa bluu na kuboresha sekta nyingine za uzalishaji.
 
Aliahidi kuwa Shirika lake litaendelea kutoa fedha kwenye maeneo ya uzalishaji na uwekezaji kupitia Wizara ya Fedha na Mipango lakini pia kuwashawishi wadau wengine kote duniani kuwekeza fedha katika maeneo mbalimbali ya uwekezaji yatakayochangia kuondoa umasikini na kutanzua changamoto zote za uzalishaji mali kupitia sekta binafsi na wajasiriamali.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Dkt. Nchemba: Serikali Kuwekeza Zaidi Kwenye Sekta Za Uzalishaji
Dkt. Nchemba: Serikali Kuwekeza Zaidi Kwenye Sekta Za Uzalishaji
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiNDO9pNE9qgxweucxgs3D4h62Bq9TcXSRag8avHqAVbZtGBfYsDHveFMblm_VIWqtpHjXOLrgrM6aqnfrAb6ceO327-GL4r09a8RFAXYBD6k-mLsUjQ0QdzVzipZnFYl3mMIt21tI0WthtWCpW37mtxTTgCWxa4D_g6Aw_fFIZNlzmAiPtgrAxqSlLWQ/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiNDO9pNE9qgxweucxgs3D4h62Bq9TcXSRag8avHqAVbZtGBfYsDHveFMblm_VIWqtpHjXOLrgrM6aqnfrAb6ceO327-GL4r09a8RFAXYBD6k-mLsUjQ0QdzVzipZnFYl3mMIt21tI0WthtWCpW37mtxTTgCWxa4D_g6Aw_fFIZNlzmAiPtgrAxqSlLWQ/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/04/dkt-nchemba-serikali-kuwekeza-zaidi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/04/dkt-nchemba-serikali-kuwekeza-zaidi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy