TRC Yasaini Mkataba Wa Ununuzi Wa Behewa 1430 Kwa Ajili Ya Reli Ya Kisasa SGR
HomeHabari

TRC Yasaini Mkataba Wa Ununuzi Wa Behewa 1430 Kwa Ajili Ya Reli Ya Kisasa SGR

SERIKALI  kwa kushirikiana na kampuni  ya CRRC International  ya China wamesaini mkataba wa ununuzi  wa mabehewa 1,430 ya  mizigo ya Reli...


SERIKALI  kwa kushirikiana na kampuni  ya CRRC International  ya China wamesaini mkataba wa ununuzi  wa mabehewa 1,430 ya  mizigo ya Reli ya kisasa- SGR mkataba huo utakaogharimu  Dola za kimarekani  milioni 127.2.

Akizungumza katika hafla hiyo Mkurugenzi Mkuu wa  Shirika la Reli Tanzania (TRC) Masanja Kadogosa, amesema mkataba huu ni wa miezi kumi na mbili na utahusisha  usanifu na utengenezaji wa Mabehewa kwa ajili ya kubeba mizigo ya aina mbalimbali kulingana na aina ya behewa na matakwa ya mteja kupitia reli ya kisasa.

Aidha Kadogosa alisema ujio wa mabehewa hayo yatasaidia kusafirisha vitu mbalimbali kama Mifugo, Sukari, Chumvi, Pamba, Tumbaku, Kahawa na magari ambayo kwa kiasi kikubwa yanasaidia kukuza biashara ndani na nje ya nchi kama Uganda.

Akizungumza katika hafla hiyo Mkurugenzi Mkuu wa  Shirika la Reli (TRC) Masanja Kadogosa amesema mkataba huu ni wa miezi kumi na mbili na utahusisha  usanifu na utengenezaji wa Mabehewa kwa ajili ya kubeba mizigo ya aina mbalimbali kulingana na aina ya behewa na matakwa ya mteja kupitia reli ya kisasa.

Aidha Kadogosa alisema ujio wa mabehewa haya yatasaidia kusafirisha vitu mbalimbali kama mifugo,sukari, chumvi, pamba, tumbako, Kahawa na magari ambazo kwa kiasi kikubwa zitasaidia kukuza biashara ndani na nje ya nchi kama Uganda, Rwanda, Burundi na congo kwa kurahisisha usafirishaji na kupunguza  gharama  za matengenezo ya barabara.

Pia Kadogosa alisema faida za mabehewa hayo ni kwamba yataraisisha biashara ya usafirishaji wa mizigo kupitia reli ya kisasa kwa umbali wa km 500, hivyo unatarajia kukamilika kwa manunuzi na kuwasili kwa mabehewa hayo February 2023.
 

Akizungumza katika Hafla hiyo leo jijini Dar es salaam Waziri wa ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame mbarawa Serikali imedhamiria kuhakikisha huduma ya usafiri wa mizigo inaimarika ndani na nje ya mipaka ya Tanzania kwa lengo la kuongeza pato la taifa na kukuza uchumi.

‘Ujenzi wa Reli ya kisasa unaoendelea hivi sasa kwa kipande cha Dar es Salaam – Morogoro ambacho kimefika 95%, Morogoro – Makutupora ambacho kimefika 81% na kipande cha Mwanza – Isaka ambacho kimefika 4% ni ishara tosha kwamba Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan imedhamiria kuongeza ufanisi na kuboresha huduma ya usafiri na usafirishaji kupitia reli’amesema Waziri Prof Mbarawa.

Aidha,Profesa Mbarawa amesema kutokana na uwezo mkubwa wa reli ya kisasa Behewa hizo zitasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza mrundikano wa mizigo katika bandari ya Dar es Salaam ambapo treni moja itakuwa na uwezo wa kubeba Tani 10,000 kwa mkupuo ambayo ni sawa na malori 500.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: TRC Yasaini Mkataba Wa Ununuzi Wa Behewa 1430 Kwa Ajili Ya Reli Ya Kisasa SGR
TRC Yasaini Mkataba Wa Ununuzi Wa Behewa 1430 Kwa Ajili Ya Reli Ya Kisasa SGR
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEjee_crUGKgBG9vLngbgdG5aCocKk_J_zpVQ14W_MsmMumOAMnrQY3ovXmbtGjGTqBgk0ZQhSZ1Wz56fbwrlkVRVG6xVCFH-_4pa1bJXInve_SQg5is4pZ5O-gAHVuBHoPHjj09V2ohvVwGeEZ2rgZ2Py9KeoGAjnTWIVAw7bpZAM7-BcKY3eWv6fAH1w=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEjee_crUGKgBG9vLngbgdG5aCocKk_J_zpVQ14W_MsmMumOAMnrQY3ovXmbtGjGTqBgk0ZQhSZ1Wz56fbwrlkVRVG6xVCFH-_4pa1bJXInve_SQg5is4pZ5O-gAHVuBHoPHjj09V2ohvVwGeEZ2rgZ2Py9KeoGAjnTWIVAw7bpZAM7-BcKY3eWv6fAH1w=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/trc-yasaini-mkataba-wa-ununuzi-wa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/trc-yasaini-mkataba-wa-ununuzi-wa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy