Rasi Samia Awaagiza Wakaguzi Wa Ndani Wa Halmashauri Kufanya Kazi Kwa Ufanisi Kuzuia Mianya Ya Ufujaji Na Matumizi Mabaya Ya Fedha
HomeHabari

Rasi Samia Awaagiza Wakaguzi Wa Ndani Wa Halmashauri Kufanya Kazi Kwa Ufanisi Kuzuia Mianya Ya Ufujaji Na Matumizi Mabaya Ya Fedha

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewaagiza Wakaguzi wa ndani wa Halmashauri kufanya kazi kwa ufanisi ili...


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewaagiza Wakaguzi wa ndani wa Halmashauri kufanya kazi kwa ufanisi ili kuzuia mianya ya ufujaji na matumizi mabaya ya fedha za miradi ya maendeleo.

Mhe. Rais Samia ametoa agizo hilo  tarehe 07 Februari, 2022 wakati akizungumza na wananchi wa Bunda mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika mradi wa miundombinu ya kusafisha na kutibu maji utakaogharimu shilingi Bilioni 10.6 utakapokamilika, katika viwanja vya Shule ya Msingi Miembeni, wilayani Bunda Mkoani Mara.

Aidha, Mhe. Rais Samia amewataka Wakaguzi hao kufanya ukaguzi wa hesabu za fedha za miradi ya maendeleo mapema na kwa kila hatua badala ya kusubiri ukaguzi kufanywa na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).

Mhe. Rais Samia pia ameitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoani Mara kuzuia vitendo vya rushwa kwa kufuatilia hatua zote za matumizi ya fedha katika miradi  pindi fedha za miradi zinapokuwa zimetolewa badala ya kungoja ripoti ya Mkaguzi wa Mahesabu ndipo wafuatilie.

Vile vile, Mhe. Rais Samia amekemea ucheleweshwaji wa miradi mbalimbali mkoani humo kutokana na ubinafsi na ubadhirifu unaofanywa na baadhi ya watendaji Serikalini.

Mhe. Rais Samia amewataka viongozi kusogeza huduma muhimu kwa wananchi na isisubiriwe hadi kufanyika kwa mgao wa maeneo ya utawala.

Aidha, Mhe.Rais Samia amewataka wale wote waliopewa nafasi za uongozi kutekeleza majukumu yao kikamilifu na kuwataka wananchi kuwaunga mkono na kushirikiana nao ili waweze kutoa huduma kikamilifu.

Mhe. Rais Samia amewaonya viongozi wa mkoa wa Mara kuwa iwapo Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa miradi ya maendeleo na fedha hizo kukaa kwa kipindi cha miezi 6 hadi mwaka bila kutumika kwa sababu za kuvutana, fedha hizo zitarudishwa Serikalini kwa matumizi mengine.

Awali akiwa njiani kuelekea Bunda, Mhe. Rais Samia amewasalimia wananchi wa eneo la Butiama na kuwaahidi wananchi hao kuwa pamoja na na miradi mbalimbali iliyotekelezwa wilayani humo Serikali itaendelea kuwaletea maendeleo zaidi.

Aidha, akiwa wilayani Butiama, Mhe. Rais Samia pia ametembelea kaburi la Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Mhe. Rais Samia amemaliza ziara ya siku nne mkoani Mara na kuwashukuru wananchi wa mkoa huo kwa mapokezi makubwa waliyompa muda wote akiwa ziarani mkoani humo.

Jaffar Haniu
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Rasi Samia Awaagiza Wakaguzi Wa Ndani Wa Halmashauri Kufanya Kazi Kwa Ufanisi Kuzuia Mianya Ya Ufujaji Na Matumizi Mabaya Ya Fedha
Rasi Samia Awaagiza Wakaguzi Wa Ndani Wa Halmashauri Kufanya Kazi Kwa Ufanisi Kuzuia Mianya Ya Ufujaji Na Matumizi Mabaya Ya Fedha
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi1I8Bnh2u-zh_klXuP5u6oGWmS8_qkvEAuQTnkMHNvTTPKz7VHhIx-W7-99rYsjAhlHZvh7b7FG7lo6XNup7d5B8y4baG5siAmf8Ppkf6MWq8zZ3OuUDMifoMUB6x8PxKaDtnrCSx9b7EBqPhOp-_gz0gxHwASmCRH2YvviAMuY5DeAjyQO_3iDk0dkg/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi1I8Bnh2u-zh_klXuP5u6oGWmS8_qkvEAuQTnkMHNvTTPKz7VHhIx-W7-99rYsjAhlHZvh7b7FG7lo6XNup7d5B8y4baG5siAmf8Ppkf6MWq8zZ3OuUDMifoMUB6x8PxKaDtnrCSx9b7EBqPhOp-_gz0gxHwASmCRH2YvviAMuY5DeAjyQO_3iDk0dkg/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/rasi-samia-awaagiza-wakaguzi-wa-ndani.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/rasi-samia-awaagiza-wakaguzi-wa-ndani.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy