Mbunge Ataka Serikali Kutenga Fedha Kukarabati Makazi Ya Wazee
HomeHabari

Mbunge Ataka Serikali Kutenga Fedha Kukarabati Makazi Ya Wazee

 MBUNGE wa Viti Maalum (CCM) Bahati Ndingo ameihoji serikali Bungeni kuhusu mpango uliopo wa kutenga fedha za ukarabati wa vituo vya waze...

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo September 14
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo September 13
Rais Samia Apangua Baraza la Mawaziri, Ateua Mwanasheria Mkuu Mpya


 MBUNGE wa Viti Maalum (CCM) Bahati Ndingo ameihoji serikali Bungeni kuhusu mpango uliopo wa kutenga fedha za ukarabati wa vituo vya wazee ambavyo vingi vimechakaa.

Bahati aliuliza swali hilo jana Bungeni kwa Naibu Waziri, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na makundi maalum, Mwanaidi Ali Khamisi.

Akijibu swali hilo, Mwanaidi alisema katika kuboresha utoaji wa huduma, serikali imeendelea kuboresha majengo na miundombinu ya makazi ya wazee kwa awamu ambapo kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2019/2020 na mwaka wa fedha 2020/2021 ukarabati umefanyika katika makazi saba ya wazee yakiwemo Nunge (Dar es Salaam), Kolandoto (Shinyanga), Njoro (Kilimanjaro), Magugu (Manyara), Kiilima (Kagera), Fungafunga (Morogoro) na Sukamahela (Singida).

Aidha, alisema serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa Makazi ya Wazee Wasiojiweza nchini kwa kadri ya upatikanaji wa rasilimali fedha.

Hata hivyo, Mbunge Bahati alipata nafasi kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza ambapo katika swali lake la kwanza alitaka kufahamu mpango wa serikali wa kuongeza idadi ya vituo vya kulelea wazee.

“Tafiti mbalimbali zimeonyesha uwepo wa ongezeko la wazee duniani, je, wizara inajipangaje kuongeza idadi ya vituo vya kulelea wazee,” alihoji.

Kadhalika, katika swali lake la pili, alihoji mpango wa serikali wa kuweka vifaa tiba katika vituo mbalimbali vya kulelea wazee.

Akijibu maswali hayo, Mwanaidi alisema kila mwaka wa fedha serikali imekuwa ikitoa fedha kuboresha mahitaji ya wazee kama mavazi, chakula na afya bora.

Alisisitiza kuwa serikali ya Rais Samia inawajali na kuwathamini wazee kwa kuhakikisha kundi hilo muhimu linapata huduma bora.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Mbunge Ataka Serikali Kutenga Fedha Kukarabati Makazi Ya Wazee
Mbunge Ataka Serikali Kutenga Fedha Kukarabati Makazi Ya Wazee
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhGE60za2R9nTSbh37VH_D4mCGKI9BXP5dBGx1A8DFD3NA-NbDlx3Q7PbEun77jDeUQjQ3Dgeoy35eH5OYIyCHNWCZhwkkKt-UQeWdOKc4xNsZNKuaVL39UMiaHJb96dwoDX6EX9OrmCVmGr5usc7rjv6mP77uQRF5bYga2Hgj2NQMjSXLAlVz00UwvKw=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhGE60za2R9nTSbh37VH_D4mCGKI9BXP5dBGx1A8DFD3NA-NbDlx3Q7PbEun77jDeUQjQ3Dgeoy35eH5OYIyCHNWCZhwkkKt-UQeWdOKc4xNsZNKuaVL39UMiaHJb96dwoDX6EX9OrmCVmGr5usc7rjv6mP77uQRF5bYga2Hgj2NQMjSXLAlVz00UwvKw=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/mbunge-ataka-serikali-kutenga-fedha.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/mbunge-ataka-serikali-kutenga-fedha.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy