Bunge Laridhia Nyongeza Ya Shilingi Trilioni 1.3 Ya Bajeti Ya Serikali Kwa Mwaka 2021/22
HomeHabari

Bunge Laridhia Nyongeza Ya Shilingi Trilioni 1.3 Ya Bajeti Ya Serikali Kwa Mwaka 2021/22

Na. Ramadhani Kissimba na Saidina Msangi, WFM, Dodoma Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limeridhia Serikali kuongeza matumizi ya ...

France pursues female suspect after deadly sieges
Msichana wa miaka kumi ajilipua Nigeria
Iraq says rebuilding of army still in early stages


Na. Ramadhani Kissimba na Saidina Msangi, WFM, Dodoma
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limeridhia Serikali kuongeza matumizi ya zaidi ya shilingi trilioni 1.3 Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2021/22 na kuifanya Bajeti hiyo kuongezeka kutoka sh. trilioni 36.66 hadi kufikia sh. trilioni 37.98.

Akiwasilisha mapendekezo ya nyongeza ya bajeti kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba(Mb), Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Mhe. Mhandisi Hamad Yusuff Masauni alisema kuwa Serikali ilipata Mkopo usio na riba kutoka Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) wenye thamani ya shilingi trilioni 1.3 sawa na dola za Marekani milioni 567.3.

Mh. Masauni alisema kuwa fedha hizo zilizopatikana hazikuwa sehemu ya bajeti iliyoidhinishwa na Bunge katika mwaka 2021/22 hivyo Serikali inawajibika chini ya kifungu cha 43 cha Sheria ya Bajeti, SURA 439 na Ibara ya 137 (2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwasilisha bungeni mapendekezo ya kuomba ridhaa ya Bunge kutumia fedha za mkopo huo.

Aliongeza kuwa fedha hizo zitatumika kuwakinga Watanzania dhidi ya maambukizi ya UVIKO-19 na kuchochea shughuli za kiuchumi na kijamii zilioathirika na ugonjwa huo kwa upande wa Tanzania Bara na Visiwani.

‘Kati ya kiasi hicho, shilingi bilioni 1,079.6 ni kwa ajili ya Tanzania Bara, sawa na dola za Marekani milioni 467.3 na shilingi bilioni 231.0, sawa na dola za Marekani milioni 100 kwa ajili ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar’ alisema Mh. Masauni.

Mhe.Masauni aliongeza kuwa mchakato wa kupata mkopo huo ulihusisha sekta mbalimbali ambapo baadhi ya sekta hazikukidhi kujumuishwa kwenye mgao wa fedha hizo kwa mujibu wa vigezo na masharti ya IMF. Aliongeza kuwa sekta zilizokidhi vigezo hivyo ni afya, elimu, utalii, maji, biashara ndogo ndogo kupitia makundi maalum ya vijana, wanawake na wenye ulemavu na kaya maskini kupitia mfuko wa hifadhi ya jamii (TASAF).

Alifafanua kuwa matumizi ya fedha hizo yamegawanywa kulingana na vipaumbele ilivyojiwekea Serikali kwa mwaka wa fedha 2021/22 ambapo sekta ya afya ilipata shilingi bilioni 466.9, sekta ya elimu shilingi bilioni 368.9, sekta ya maji shilingi bilioni 139.4,sekta ya utalii shilingi bilioni 90.2, TASAF shilingi bilioni 5.5 kwa ajili ya kuwezesha kaya masikini 34,375 na eneo lingine lililopatiwa fedha ni makundi maalum ambao wamepatiwa shilingi bilioni 5, pamoja na timu ya uratibu, ufuatiliaji na tathmini waliopewa shilingi bilioni 3.7.

Aliwahakikishia Wabunge kuwa fedha hizo zitatumika na kusimamiwa kikamilifu na Serikali na kumtaka Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) kufatilia matumizi ya fedha hizo ili kuzuia ubadhilifu wakati wa utekelezaji wa miradi ilianishwa kutekelezwa kwa kutumia fedha hizo.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Bunge Laridhia Nyongeza Ya Shilingi Trilioni 1.3 Ya Bajeti Ya Serikali Kwa Mwaka 2021/22
Bunge Laridhia Nyongeza Ya Shilingi Trilioni 1.3 Ya Bajeti Ya Serikali Kwa Mwaka 2021/22
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgy1QPn8cnuMT6fghIep5j_ZQADrjGWAUmxb2oM8jN8XKVhUtoW9PoAOEdrjdnqx7MR4iBbGDIic5JiWx-fJQz34Z7JL_4o1x8wdgwFx2rzd8GZ4OY5H3_wTqT5uQxidGc5l35rxE-b6llUF0hYCsh7Au6paZMG3SYXvnEg1PI3h8NcDCkVQo0eGzS19A=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgy1QPn8cnuMT6fghIep5j_ZQADrjGWAUmxb2oM8jN8XKVhUtoW9PoAOEdrjdnqx7MR4iBbGDIic5JiWx-fJQz34Z7JL_4o1x8wdgwFx2rzd8GZ4OY5H3_wTqT5uQxidGc5l35rxE-b6llUF0hYCsh7Au6paZMG3SYXvnEg1PI3h8NcDCkVQo0eGzS19A=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/bunge-laridhia-nyongeza-ya-shilingi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/02/bunge-laridhia-nyongeza-ya-shilingi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy