Waziri Mkuu wa Sudan Minister Abdalla Hamdok ametangaza kujiuzulu wiki chache baada ya kurejeshwa madarakani katika mkataba wenye utata...
Waziri Mkuu wa Sudan Minister Abdalla Hamdok ametangaza kujiuzulu wiki chache baada ya kurejeshwa madarakani katika mkataba wenye utata na majeshi.
Wanajeshi walichukuwa madaraka Mwezi Oktoba na kumweka Bw.Hamdok chini ya kifungo cha nyumbani, lakini akarejeshwa madarakani baada ya kufikia mkataba wa kugawana na kiongozi wa mapinduzi.
Waandamanaji walipinga makubaliano hayo, wakishinikiza utawala kamili wa kisiasa na kiraia.
Kujiuzulu kwake kunafuatia siku nyingine ya maandamano, ambapo madaktari walisema takribani watu wawili waliuawa.
Katika hotuba iliyooneshwa kwenye televisheni,Bw. Hamdok alisema Sudan iko katika "kipindi hatari ambacho kinatishia ustawi wake kwa jumla ".
Alisema alijaribu kila awezalo kuzuia nchi "kutumbukia kwenye janga ", lakini "licha ya yote yaliyofanywa kufikia uwiano... hilo halijafanyika ".
" Niliamua kurudisha jukumu hilo na kutangaza kujiuzulu uwaziri mkuu, na kutoa nafasi kwa mwanaume au mwanamke mwingine wa nchi hii adhimu ili... kuisaidia kupita kile kilichosalia cha kipindi cha mpito kwa nchi kuelekea utawala wa kidemokrasia ya kiraia," aliongeza kusema.
Credit: MPEKUZI
Thanks for your time please share with your friends
COMMENTS