Serikali Yatenga Bilioni Mbili Kutekeleza Mradi Wa Maktaba Mtandao
HomeHabari

Serikali Yatenga Bilioni Mbili Kutekeleza Mradi Wa Maktaba Mtandao

Serikali imetenga jumla ya Shilingi bilioni 2 kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa Maktaba Mtandao ili kuongeza wigo wa upatikanaji huduma za...


Serikali imetenga jumla ya Shilingi bilioni 2 kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa Maktaba Mtandao ili kuongeza wigo wa upatikanaji huduma za maktaba kutokana na ongezeko la idadi ya watumiaji wa huduma hiyo nchini.

Hayo yamesemwa  Januari 3, 2022 Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako (Mb) wakati akizindua Bodi ya Wakurugenzi ya Bodi ya Huduma za Maktaba Tanzania (BOHUMATA) ambapo amesema fedha hizo ni sehemu ya Shilingi bilioni 10.5 za bajeti ya maendeleo ya Bodi hiyo zilizotolewa na Serikali katika mwaka wa fedha 2021/22.

Aidha ameitaka Bodi hiyo kuhakikisha katika utafutaji wa machapisho na vitabu izingatie kupata vitabu vinavyolenga kukuza ujuzi, maarifa na stadi mbalimbali kwa Watanzania wote wakiwemo wenye mahitaji maalum.

“Nitoe rai kwa Bodi kuhakikisha mnatafuta machapisho na vitabu vinavyolenga kukuza ujuzi, maarifa na stadi mbalimbali. Tunataka maktaba iwe kwa Watanzania wote yaani watoto, wajasiriamali, walemavu wa aina mbalimbali, wakulima, wafugaji, watafiti wote waweze kupata huduma hii muhimu,” amesisitiza Waziri Ndalichako.

Katika hatua nyingine Waziri Ndalichako amewataka wajumbe wa bodi hiyo kupitia Sheria ya Bodi Na. 6 ya mwaka 1975 na kumshauri iwapo inafaa kuendelea kutumika au inahitaji maboresho ili kwendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia nchini na ulimwenguni kwa ujumla.

“Niwape changamoto kuwa Sheria hii ni ya muda mrefu hivyo pamoja na kuitumia kutekeleza majukumu yenu, nategemea kabla Bodi haijamaliza muda wake inipe mapendekezo iwapo sheria hii bado inakidhi au kuna haja ya kuifanyia mapitio ili iendane na teknolojia ya wakati huu,” amesema Prof. Ndalichako.

Akiongea katika uzinduzi huo Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Prof. Rwekaza Mukandala amesema wamepewa dhamana kubwa na Taifa ya kuiongoza Bodi hiyo na kuahidi kutekeleza jukumu hilo kwa umakini, uadilifu na weledi.

Amesema Wajumbe wa Bodi hiyo wanatoka katika nyanja mbalimbali na wana uzoefu wa kutosha na umahiri hivyo anaamini watakuwa na mchango mkubwa utakaoiwezesha Taasisi hiyo kutoa huduma bora na za kisasa kwa wananchi na hivyo kuchangia maendeleo.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa BOHUMATA, Dkt. Mboni Ruzegea amesema Bodi hiyo inakusudia kufanya mabadiliko na upangaji upya wa shughuli na huduma za Taasisi hiyo ili kwendana na dira na dhima ya taasisi katika kutekeleza Mpango Mkakati wa miaka mitano 2020/21 – 2024/25.

Amesema Mpango huo unalenga utoaji wa huduma za kisasa za maktaba kwa njia ya kidigitali, utawala na usimamizi wa rasilimali watu na kuimarisha uwezo wa Taasisi katika kutoa huduma kwa wananchi.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Serikali Yatenga Bilioni Mbili Kutekeleza Mradi Wa Maktaba Mtandao
Serikali Yatenga Bilioni Mbili Kutekeleza Mradi Wa Maktaba Mtandao
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgys2yx0e3unaCLBCyg7eLNMZ8hvPBTO8Ab1imMyDYSGNrKMH4YBhxyWjNOMM9CTTEfPA-M2oVacadIptKLlS8VoZITpqEHwRNgind4GBgdqkIKtY6OzTVYJd9BSuKARgxr2TlsnT2ir6wqB7wiSBHHrThZ9hmZVvoevWna1Qi8Q0u-y_rO4uQT2pklqA=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEgys2yx0e3unaCLBCyg7eLNMZ8hvPBTO8Ab1imMyDYSGNrKMH4YBhxyWjNOMM9CTTEfPA-M2oVacadIptKLlS8VoZITpqEHwRNgind4GBgdqkIKtY6OzTVYJd9BSuKARgxr2TlsnT2ir6wqB7wiSBHHrThZ9hmZVvoevWna1Qi8Q0u-y_rO4uQT2pklqA=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2022/01/serikali-yatenga-bilioni-mbili.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2022/01/serikali-yatenga-bilioni-mbili.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy