Serikali Yapokea Dozi 376,320 Za Moderna
HomeHabari

Serikali Yapokea Dozi 376,320 Za Moderna

Na WAMJW-DSM Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imepokea Dozi 376,320 za Moderna ikiwa ni mwen...


Na WAMJW-DSM
Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imepokea Dozi 376,320 za Moderna ikiwa ni mwendelezo wa mkakati wa Serikali ya awamu ya sita kuhakikisha ikiwakinga Wananchi wake dhidi ya ugonjwa wa UVIKO-19.

Hafla fupi ya mapokezi imefanyika 24 Disemba 2021 na kuongozwa na Waziri wa Afya Dkt. Dorothy Gwajima katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na baadhi ya viongozi wa Serikali, Ubalozi na Taasisi zisizo za kiserikali.

Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Gwajima amesema, Serikali kupitia Wizara ya Afya imelenga kuwakinga jumla ya Watanzania 249,795 kutokana na kupokea Chanjo dozi 376,320 za Moderna zilizoingia kupitia mpango wa COVAX Facility zitakinga watanzania 188,160 ikiwa ni awamu ya kwanza kupokea aina ya Chanjo za Moderna.

"Mapokezi ya chanjo hizi za leo yanafanya jumla ya chanjo tulizopokea hapa nchini tangu tuanze kutoa chanjo za chanjo dhidi ya UVIKO 19 hadi sasa zimefikia dozi 6,408,950 zikijumuisha (Sinopharm, Janssen, Pfizer), na leo Moderna ambazo zinatosha kuchanja jumla ya watanzania 3,204,475
hivyo niwaombe wanaohusika na zoezi hilo kuwajibika kwa kasi kubwa ili kuwawezesha watanzania wengi kupata chanjo mapema iwezekanavyo amesema Mhe.Dkt Gwajima.

Aidha,Mhe.Dkt.Gwajima amesema kuwa Wizara imetoa Mwongozo wa Chanjo unaofafanua vyema taratibu za utoaji wa chanjo hizi wenye lengo la kufikia uchanjaji wa asilimia 60 ya watanzania ili kudhibiti ugonjwa wa uviko 19.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Serikali Yapokea Dozi 376,320 Za Moderna
Serikali Yapokea Dozi 376,320 Za Moderna
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEi3eoiyfPBofE9kBuutltCqy1PCB_WtxS4l1y5njhK2SVA1QJFAhltzzZPrN7w3t6ExHoq7WYj9LzT-WwllJVLP24kg5ct1g-QsUnA66UsupMcKZbPA7sFNfG15TUtUKjtmFrZ1wYDZxZLVa_GkohRWULAPa-II4iB_piWayQgNDMpptLdRXVOcSXcnDA=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEi3eoiyfPBofE9kBuutltCqy1PCB_WtxS4l1y5njhK2SVA1QJFAhltzzZPrN7w3t6ExHoq7WYj9LzT-WwllJVLP24kg5ct1g-QsUnA66UsupMcKZbPA7sFNfG15TUtUKjtmFrZ1wYDZxZLVa_GkohRWULAPa-II4iB_piWayQgNDMpptLdRXVOcSXcnDA=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/serikali-yapokea-dozi-376320-za-moderna.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/serikali-yapokea-dozi-376320-za-moderna.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy