Serikali Itaendelea Kuunga Mkono Juhudi Za Mashirika Yasiyokuwa Ya Kiserikali (Ngos)
HomeHabari

Serikali Itaendelea Kuunga Mkono Juhudi Za Mashirika Yasiyokuwa Ya Kiserikali (Ngos)

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Dkt. Selemani Jafo amesema Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi z...


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Dkt. Selemani Jafo amesema Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za Mashirika yasiyokuwa ya Kiserikali (NGOs) katika shughuli za uhifadhi wa mazingira.

Dkt. Jafo ametoa kauli hiyo  Desemba 17, 2021 wakati akifungua Kongamano la Kukomboa Ardhi iliyochakaa katika Nyanda kame za Tanzania sanjari na Maadhimisho ya miaka 10 ya Shirika la Lead Foundation.

Alisema kuwa kongamano hilo linatoa taswira ya namna gani NGOs zinashiriki kikamilifu katika kusukuma mbele agenda ya mazingira nchini hivyo kuwajengea uelewa kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kulinda na kuhifadhi mazingira.

“Niliwahi kuitisha mkutano na mashirika yanayojihusha na suala zima mazingira na leo najisikia faraja kubwa kuona mashirika haya yanapiga hatua na lengo langu kubwa ni kuona kila mmoja anshiriki katika suala zima la uhifadhi wa mazingira,” alisema.

Aidha Waziri Jafo alisema Serikali itaendelea kusimamia Kampeni Kabambe ya Hifadhi na Usafi wa Mazingira inayowashirikisha wadau mbalimbali wakiwemo wadau kutoka mashirika hayo.

Alisema anafarijika kutokana na Mpango Mkakati wa miaka 10 uliozinduliwa na Lead Foundation ambao unaonesha namna gani linaunga mkono Serikali katika hatua za kutunza na kuhidhi mazingira hususan katika eneo la mabadiliko ya tabianchi linaloikabili dunia.

Kwa upande mwingine alitumia nafasi hiyo kuwa kutoa rai kwa wanachi kutumia kipindi hiki cha masika kupanda miti kwa wingi na kuitunza ili kukabiliana na ukame ambao huleta athari mbalimbali za kijamii.

Aliwaelekeza wakuu wa mikoa na wilaya kusimamia vizuri zoezi hilo na kuhakikisha misitu haichomwi ovyo ili kuepusha athari za mabadiliko ya tabianchi zinazochangia kukosekana kwa mvua.

Akitoa shukrani, Mwanzilishi wa Shirika la Lead Foundation, Askofu mstaafu Dkt. Simon Chiwanga alisema kazi ya ukumbozi wa mazingira inafanywa kwa namna mbili ambazo ni kuelimisha na kumbadilisha mtu fikra.

Alisema kupitia uwasilisha wa elimu ya mazingira unaofanywa na Waziri Jafo Dkt. Jafo ni wa kipekee na unaweza kubadilisha fikra za wananchi kuona umuhimu wa kushiriki kuhifadhi mazingira.

“Nafurahia sana uwepo wako hapa mheshimiwa waziri na hiyo ‘passion’, hiyo huruma na upendo ulio nao tunamuomba Mungu akubariki sana,” alisema Askofu mstaafu Chiwanga


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Serikali Itaendelea Kuunga Mkono Juhudi Za Mashirika Yasiyokuwa Ya Kiserikali (Ngos)
Serikali Itaendelea Kuunga Mkono Juhudi Za Mashirika Yasiyokuwa Ya Kiserikali (Ngos)
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhHKQ0V7BXQmE4t_gJa2sKwkBR6nXpndEWc6e5dXDr9LuFchzdCQE4gOWP9_vSAS7vchSr0ZNpFIThFHZmbzDhWIM9Juc0mZkeDsRJOrv1zdNPYgxInT88tJti1MGB6l44Hc1-qM48LbSrtXfyZWLHO-1qO-2yt_YOK3iikZh4VfX_8UpFsaV4BnknFHw=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEhHKQ0V7BXQmE4t_gJa2sKwkBR6nXpndEWc6e5dXDr9LuFchzdCQE4gOWP9_vSAS7vchSr0ZNpFIThFHZmbzDhWIM9Juc0mZkeDsRJOrv1zdNPYgxInT88tJti1MGB6l44Hc1-qM48LbSrtXfyZWLHO-1qO-2yt_YOK3iikZh4VfX_8UpFsaV4BnknFHw=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/serikali-itaendelea-kuunga-mkono-juhudi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/12/serikali-itaendelea-kuunga-mkono-juhudi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy