Rais Samia Kufungua Mkutano Wa Taasisi Za Fedha Nchini
HomeHabari

Rais Samia Kufungua Mkutano Wa Taasisi Za Fedha Nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufungua mkutano wa 20 wa Taasisi za Fedha nchini utakaofany...

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufungua mkutano wa 20 wa Taasisi za Fedha nchini utakaofanyika jijini Dodoma, tarehe 25 na 26 Novemba 2021, utakaojadili uimarishaji wa uchumi wa Tanzania kufuatia janga la UVIKO-19.

Mkutano huo, ambao umeandaliwa na Benki Kuu ya Tanzania kwa kushirikiana na Umoja wa Mabenki nchini (TBA), unatarajiwa kuhudhuriwa na washiriki takribani 300 kutoka taasisi za fedha, sekta binafsi, serikali, mashirika ya kimataifa, taasisi za elimu, asasi za kiraia na vyombo vya habari.

Mada nne zitawasilishwa na wataalam waliobobea kutoka ndani na nje ya nchi, ambazo ni:

∙ Ukuaji wa uchumi endelevu wakati na baada ya janga la UVIKO -19: Vipaumbele na sera mbadala;

∙ Kuchochea kasi ya maendeleo ya kidijitali katika kuimarisha ukuaji endelevu wa uchumi;

∙ Sarafu za kidijitali: Uzoefu, vihatarishi na usimamizi; na

∙ Kuongeza mikopo kwa sekta binafsi baada ya janga la UVIKO-19: Wajibu wa Serikali, taasisi za fedha na sekta binafsi.

Mada hizo zimechaguliwa kuendana na hali ya sasa, ambapo uchumi wa dunia unaendelea kuimarika kufuatia athari za janga la UVIKO-19, na kuongezeka kwa matumizi ya teknolojia za kidijitali na fedha za mtandaoni.

Mikutano ya Taasisi za Fedha ilianzishwa na Benki Kuu ya Tanzania mwaka 1980 na imekuwa ikifanyika kila baada ya miaka miwili. Mkutano wa 19 wa Taasisi za Fedha ulifanyika jijini Dar es Salaam mwezi Novemba 2019.

Imetolewa na :

Idara ya Uhusiano wa Umma na Itifaki

 BENKI KUU YA TANZANIA



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Rais Samia Kufungua Mkutano Wa Taasisi Za Fedha Nchini
Rais Samia Kufungua Mkutano Wa Taasisi Za Fedha Nchini
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEiYtpEpSzyRtZ4a0qvF602blOrjMVThaioDRM-JdPvMV_7iUzJmABV1ulcm--RMhoOhEW10zPBAUoHKDolf85b4k4bzxJ1Nu4vc-c_HirKZmFMvXxw9UpWlHl6dyGcZ3-40YQgl9Olt0aZVDrp0ZPAoTW80ttZCPFvY3TxVtCF-W2TUGi0ceVs5BZLwtg=s16000
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEiYtpEpSzyRtZ4a0qvF602blOrjMVThaioDRM-JdPvMV_7iUzJmABV1ulcm--RMhoOhEW10zPBAUoHKDolf85b4k4bzxJ1Nu4vc-c_HirKZmFMvXxw9UpWlHl6dyGcZ3-40YQgl9Olt0aZVDrp0ZPAoTW80ttZCPFvY3TxVtCF-W2TUGi0ceVs5BZLwtg=s72-c
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/11/rais-samia-kufungua-mkutano-wa-taasisi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/11/rais-samia-kufungua-mkutano-wa-taasisi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy