KOCHA POLISI TANZANIA ACHEKELEA USAJILI WA METACHA MNATA
HomeMichezo

KOCHA POLISI TANZANIA ACHEKELEA USAJILI WA METACHA MNATA

 KOCHA Mkuu wa Polisi Tanzania, Malale Hamsini, ameweka wazi kuwa usajili bora wa vijana walioufanya akiwemo mlinda mlango, Metacha Mnata,...


 KOCHA Mkuu wa Polisi Tanzania, Malale Hamsini, ameweka wazi kuwa usajili bora wa vijana walioufanya akiwemo mlinda mlango, Metacha Mnata, ndiyo sababu ya kuwa na timu bora ambayo anaamini itawashangaza wengi msimu huu.


Metacha aliyesajiliwa na Polisi Tanzania baada ya kuachwa na Yanga, tayari amedaka katika mechi mbili za Polisi Tanzania na zote wameshinda.


Malale amesema kuwa kupata kwao ushindi kwenye mechi za mwanzo ni jambo ambalo wanahitaji kuona likiendelea hivyo watazidi kupambana kuwa imara.

 “Tunashukuru kwa kuanza msimu vizuri na kufanikiwa kushinda michezo miwili ya kwanza, kwangu haya ni matokeo ya kufanya usajili mzuri hasa wa vijana wadogo na wenye uwezo mkubwa kama kipa wetu Metacha Mnata.


“Kutokana na uwepo wa vijana wengi kwenye kikosi chetu, unaweza kuona timu imekuwa na kasi kubwa, ukiangalia mabao yote manne tuliyofunga katika michezo miwili iliyopita ilitokana na uwezo mkubwa wa kufanya mashambulizi ya kushitukiza, naamini kama tutaendelea hivi basi tunaweza kumaliza nafasi nzuri zaidi msimu huu.”


Mechi ya kwanza walishinda kwa mabao 2-0 dhidi ya KMC Uwanja wa Karatu na ule wa pili waliibuka wababe mbele ya Azam FC, Uwanja wa Ushirika Moshi kwa mabao 2-1.



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: KOCHA POLISI TANZANIA ACHEKELEA USAJILI WA METACHA MNATA
KOCHA POLISI TANZANIA ACHEKELEA USAJILI WA METACHA MNATA
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEjtdT1Hok8_EY_TTzZJVnJMGYRLv_YDVKJPH8dnqR_6KjLVJgI8k0UWSmhIEmUZP7r1p_AifKEI5Cpfg6jJWy6p8G2N9a7xjB6fU7l1e3U36oSUvCk0UHAEczzcWJ2lNMurr95NfKLybIHBsr6AWs6RKIIUwlWbJdpi_FrgssXcdY9sAGjzeSXCyVeYig=w512-h640
https://blogger.googleusercontent.com/img/a/AVvXsEjtdT1Hok8_EY_TTzZJVnJMGYRLv_YDVKJPH8dnqR_6KjLVJgI8k0UWSmhIEmUZP7r1p_AifKEI5Cpfg6jJWy6p8G2N9a7xjB6fU7l1e3U36oSUvCk0UHAEczzcWJ2lNMurr95NfKLybIHBsr6AWs6RKIIUwlWbJdpi_FrgssXcdY9sAGjzeSXCyVeYig=s72-w512-c-h640
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/kocha-polisi-tanzania-achekelea-usajili.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/10/kocha-polisi-tanzania-achekelea-usajili.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy