Serikali Yawataka Mabalozi Wanaokwenda Mahakamani Kufuatilia Kesi Ya Freeman Mbowe kufuata sheria
HomeHabari

Serikali Yawataka Mabalozi Wanaokwenda Mahakamani Kufuatilia Kesi Ya Freeman Mbowe kufuata sheria

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula amekutana kwa mazungumzo na Mabalozi,Wakuu wa Taasisi...

Picha: Rais Samia ahudhuria uzinduzi wa Utalii wa Kasa Kizimkazi, Visiwani Zanzibar
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 24, 2024
Wazazi pelekeni vijana wenu shule – Majaliwa


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula amekutana kwa mazungumzo na Mabalozi,Wakuu wa Taasisi na Mashirika ya Kimataifa yaliyopo hapa Nchini kwa lengo la kuwapa mrejesho kuhusu Mkutano wa 41 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC.

Akizungumza na Mbalozi,Wakuu wa Taasisi na Mashirika ya Kimataifa Balozi Mulamula amesema Wakuu wa Nchi na Serikali katika mkutano uliofanyika Lilongwe Malawi 17 -18,Agosti,2021 kwa pamoja walikubaliana kuendelea kukabiliana na janga la UVIKO -19 ikiwa ni pamoja na kushawishi Kampuni zinazozalisha chanjo kutoa kibali ili teknolojia yao itumike kuzalisha chanjo hizo katika Nchi zinazoendelea kurahisha upatikanaji wa chanjo hiyo kwa wote na kwa bei nafuu.

Pia amewaeleza Mabalozi,Wakuu wa Taasisi na Mashirika  kuhusu ombi la Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC kuzisihi Taasisi za fedha za Kimataifa pamoja na Nchi zilizoendelea kutoa msamaha au kurefusha muda wa urejeshwaji wa mikopo hadi pale janga hili la UVIKO 19 litakapopatiwa ufumbuzi.

Kuhusu ushiriki wa Tanzania katika mpango wa SADC wa kupeleka Jeshi katika jimbo la Cabo Delgado nchini Msumbiji Balozi Mulamula amesema suala la ulinzi na usalama kwa nchi za SADC ni ulinzi na usalama kwa Tanzania,hivyo Tanzania imeshiriki kikamilifu kwa kutoa mchango wake wa fedha pamoja na jeshi.

Pia Balozi Mulamula ametoa msisitizo kwa Mabalozi wanaokwenda Mahakamani kufuatilia mwenendo wa kesi ya Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Bw. Freeman Mbowe kufuata sheria na taratibu za Kimataifa kuhusu masuala ya Kidiplomasia ili kujiepusha na ukiukwaji wa sheria na taratibu hizo.

Balozi Mulamula amefafanua kuwa Serikali haina lengo la kuwazuia Mabalozi hao kwenda mahakamani kufuatilia kesi hiyo,lakini kutokana na na uwepo wa janga la UVIKO -19 pamoja na msongamano ni muhimu kuchukua tahadhari ikiwa ni pamoja na  kufuatilia shauri hilo kwa njia nyingine ikiwemo kupitia vyombo vya habari.

Amesisitiza kuwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ndio yenye jukumu la kuhakikisha usalama wa Wanadiplomasia waliopo hapa nchini. Hata hivyo,kwa siku za hivi karibuni baadhi ya Wanadiploamasia hao wameonekana mahakamani bila kufuata sheria,kanuni na taratibu zinazosimamia masuala ya Kidiplomasia ikiwemo kutoa taarifa kwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Kiongozi wa Mabalozi waliopo hapa Nchini Dkt. Ahamada El Badaoui amesema ulinzi wa Mabalozi waliopo hapa Nchini ni muhimu sana na kuongeza kuwa endapo kuna mabalozi wanafanya hivyo ni vyema wakafuata taratibu na sharia zilizopo jambo lililoungwa mkono na Balozi wa Zambia hapa Nchini Mhe. Benson Keith Chali.

Katika Mkutano huo baadhi ya Mabalozi wamepongeza mafanikio yaliyopatikana na kueleza kuridhishwa na namna Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan inavyoendesha shughuli zake pamoja na namna inavyotatua changamoto mbalimbali.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Serikali Yawataka Mabalozi Wanaokwenda Mahakamani Kufuatilia Kesi Ya Freeman Mbowe kufuata sheria
Serikali Yawataka Mabalozi Wanaokwenda Mahakamani Kufuatilia Kesi Ya Freeman Mbowe kufuata sheria
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgU6_tkcGiqstRYw7gNSpf_uiSpItIgCVa7Q1l2GhPTHpP5UvZOg0hYDih3FKweuvRclpOLFltbaCRGEK6V_h3gsBs2ns094pdSAxMweP_xS7Sd8SEPSRT9nRI940xkHpNAvbnGo25_0UpM/s16000/1.png
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgU6_tkcGiqstRYw7gNSpf_uiSpItIgCVa7Q1l2GhPTHpP5UvZOg0hYDih3FKweuvRclpOLFltbaCRGEK6V_h3gsBs2ns094pdSAxMweP_xS7Sd8SEPSRT9nRI940xkHpNAvbnGo25_0UpM/s72-c/1.png
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/serikali-yawataka-mabalozi-wanaokwenda.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/08/serikali-yawataka-mabalozi-wanaokwenda.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy