YANGA KUMALIZANA NA KIPA HUYU WA BURUNDI
HomeMichezo

YANGA KUMALIZANA NA KIPA HUYU WA BURUNDI

  YANGA imepania kufanya kweli katika usajili msimu huu, hiyo ni baada ya kukamilisha usajili wa Shabani Djuma, sasa klabu hiyo ipo katika...

VIDEO: MASAU BWIRWE, TUMEPARURWA SANA, INAHITAJI MUDA ILI NIJE KUELEZA KIUFASAHA
DJUMA BEKI WA AS VITA AKUBALI KUTUA YANGA
VIDEO: SIMBA YAMPA POLE MASAU BWIRE, AKUBALI MATOKEO

 YANGA imepania kufanya kweli katika usajili msimu huu, hiyo ni baada ya kukamilisha usajili wa Shabani Djuma, sasa klabu hiyo ipo katika mazungumzo ya mwisho na kipa wa Aigle Noir ya nchini Burundi, Erick Johola.

 

Johola, licha ya kucheza katika Ligi Kuu ya Burundi, lakini ni Mtanzania ambapo kipa huyo alidaka katika mchezo wa kilele cha Wiki ya Mwananchi msimu uliopita na katika mchezo huo licha ya kuonyesha kiwango kikubwa, Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 2-0.

 

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Injinia Hersi Said, aliweka wazi kuwa nchini Burundi katika Klabu ya Aigle Noir, wametengeneza urafiki mzuri sana kwa kuingia makubaliano ya baadhi ya mambo, hivyo watu wasishangae kuona wanasajili mchezaji kutoka katika klabu hiyo ambaye tayari walishamfanyia skauti na wamevutiwa naye.

 

“Burundi tumetengeneza urafiki mzuri na Klabu ya Aigle Noir na tumekubaliana katika ushirikiano wa baadhi ya mambo na tumevutiwa na mchezaji mmoja, kwa hiyo msishangae kuona kuwa tumesajili mchezaji kutoka hapo.

 

"Tumefanya skauti ya kutosha nchini Burundi, kama ambavyo mnafahamu ni nchi jirani na baada ya mchezo wetu dhidi yao tulikubaliana kushirikiana katika mambo ya maendeleo ambayo ni pamoja na haya ya usajili,” alisema kiongozi huyo.

 

Akizungumza na Championi Ijumaa, Johola alikubali kuwa yupo katika mazungumzo na uongozi wa Yanga ambao unahitaji huduma yake huku yeye akiweka wazi kuwa yupo tayari kujiunga na Yanga iwapo watafikia katika makubaliano mazuri.

 

“Ni kweli nipo katika mazungumzo na uongozi wa Yanga, wao wameonyesha kuhitaji saini yangu ili niweze kuitumikia, hivyo ndivyo ninavyoweza kukuambia na kama mazungumzo yetu ambayo bado hajakamilika yatafanikiwa kukamilika, basi nitakuwa tayari kujiunga na Yanga,” alisema kipa huyo.


Leo Julai 19 dirisha la usajili limefunguliwa na linatarajiwa kufungwa Agosti 31.



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: YANGA KUMALIZANA NA KIPA HUYU WA BURUNDI
YANGA KUMALIZANA NA KIPA HUYU WA BURUNDI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEijRTilyANHv1PhtMI9PiRy9JRsbdw1j7c7bOjUfqhnkTcgH77ZvrVc6NmXrty9MVC475-bkU5fpBZkW6vTt7Xn7JRMDRyT7TgE6VhTyYmWpDCUl9UZrwgB29c8bMVM6YFEQD8UvOvlUWsL/w640-h360/Johola.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEijRTilyANHv1PhtMI9PiRy9JRsbdw1j7c7bOjUfqhnkTcgH77ZvrVc6NmXrty9MVC475-bkU5fpBZkW6vTt7Xn7JRMDRyT7TgE6VhTyYmWpDCUl9UZrwgB29c8bMVM6YFEQD8UvOvlUWsL/s72-w640-c-h360/Johola.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/07/yanga-kumalizana-na-kipa-huyu-wa-burundi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/07/yanga-kumalizana-na-kipa-huyu-wa-burundi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy