Waziri Ummy Atoa Siku 7 Kwa Vyombo Vya Usalama Kuchunguza Vifo Vya Wanafunzi Watatu Mpwapwa
HomeHabari

Waziri Ummy Atoa Siku 7 Kwa Vyombo Vya Usalama Kuchunguza Vifo Vya Wanafunzi Watatu Mpwapwa

Nteghenjwa Hosseah, Mpwapwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Ummy Mwalimu ametoa siku 7 kwa vyombo...

Mwanza Yazizima.....Vilio,huzuni,simanzi Vyatawala Mapokezi Ya Mwili Wa Hayati Dkt.Rais Magufuli
Live Mwanza: Mwili Wa Dkt. Magufuli Ukielekea CCM Kirumba Kuagwa
Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo March 24


Nteghenjwa Hosseah, Mpwapwa
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Ummy Mwalimu ametoa siku 7 kwa vyombo vya Ulinzi na Usalama kuchunguza vifo vya wanafunzi 3 waliofariki kwa kufunikwa na kifusi katika Shule ya Msingi Mbori, Kata ya Motondo Wilayani Mpwapwa.

Wakati huo huo Mhe. Ummy amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kuwaondoa Walimu wote wa shule ya Msingi Mbori kupisha uchunguzi unaondelea.

Waziri Ummy ametoa kauli hiyo wakati aliposhiriki kuaga Miili ya wanafunzi 3 waliofariki kwenye ajali ya kufukiwa na Mchanga katika shule ya Msingi Mbori tarehe 27.07.2021.

Akiwa shuleni hapo Waziri Ummy amelaani vikali Vitendo vya Walimu kuwafanyisha kazi siziso stahili za wanafunzi tofauti na ilivyoelekezwa kwenye Waraka wa Elimu bila Malipo No. 3 wa Mwaka 2016.

Amesema “ Hatukatazi mwanafunzi kufanya kazi zinazomjenga kama vile Stadi za kazi lakini sio kumfanya mwanafunzi kama Kibarua unawezaje kumwambia mtoto akachimbe mchanga wa kujengea au akaponde kokoto tena bila Uangalizi wa Walimu “ Alihoji

Katika Shule ya Msingi Mbori tumeleta sh. Mil.12 kwa ajili ya Ujenzi wa Choo na fedha za mchanga zimejumlishwa humo inakuwaje walimu watume watoto kwenda kuchimba mchanga wa mtoni,  kuna uzembe hapa umefanyika na tutachukua hatua.

Pia Waqziri Ummy aliwataka Wakuu wa shule zote Nchini na walimu wa ujumla kuacha kuwatumikisha wanafunzi wawapo shuleni na wazingatie Waraka wa Elimu bila Malipo no 3. wa mwaka 2016 ambao unatoa ufafanuzi wa kina wa jukumu la kila mdau wa Elimu.

“Jukumu la Ujenzi wa Miundombinu ya shule ni la Wazazi pamoja na Jamii inayozunguka na sio wanafunzi, Walimu na Kamati za shule mnatakiwa kuhamaisha Wazazi na jamii kujitolea kujenga miundombinu hiyo na sio kutumikisha wanafunzi” alisistiza Waziri Ummy.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa Mhe.Josephat Maganga  amesema watoto waliofariki kwenye ajali ya kufukiwa na kifusi shuleni hapo ni watatu ambao ni Isaya Lucas Hamis, Rehema Alex na Daud Enock Mchea na watoto wengine watano walijeruhiwa wametibiwa na kuruhusiwa kurejea majumbani kwao.

Tukio la Watoto kufukiwa na kifusi lilitokea Tarehe 27.07.2021 katika Shule ya Msingi Mbori iliyopo Kata ya Matomondo Wilayani Mpwapwa baada ya watoto hao kupewa kazi na walimu wao kuchimba mchanga kwa ajili ya ujenzi wa choo unaondelea shuleni hapo.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Waziri Ummy Atoa Siku 7 Kwa Vyombo Vya Usalama Kuchunguza Vifo Vya Wanafunzi Watatu Mpwapwa
Waziri Ummy Atoa Siku 7 Kwa Vyombo Vya Usalama Kuchunguza Vifo Vya Wanafunzi Watatu Mpwapwa
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjUwqTQ-AeiddlGNHo3tmQzmJzBOirG6g0WROUWWs2uirtEmBcWMSRAhPHI6Y5nJdgrTR86T5HV3fpXPP2Bf4Zqc780NL5wfcODIqM9v6_MmxFqhRiad24E7u8Q0FqoqGvm9nt0qpc9R9bs/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjUwqTQ-AeiddlGNHo3tmQzmJzBOirG6g0WROUWWs2uirtEmBcWMSRAhPHI6Y5nJdgrTR86T5HV3fpXPP2Bf4Zqc780NL5wfcODIqM9v6_MmxFqhRiad24E7u8Q0FqoqGvm9nt0qpc9R9bs/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/07/waziri-ummy-atoa-siku-7-kwa-vyombo-vya.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/07/waziri-ummy-atoa-siku-7-kwa-vyombo-vya.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy