SAWA KOMAA, LAKINI MANARA, BARBARA CHONDE
HomeMichezo

SAWA KOMAA, LAKINI MANARA, BARBARA CHONDE

Na Saleh Ally UKIACHANA na suala la kuchukua  ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara mara  nne mfululizo katika kipindi hiki, moja ya  sifa kub...


Na Saleh Ally

UKIACHANA na suala la kuchukua ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara mara nne mfululizo katika kipindi hiki, moja ya sifa kubwa kabisa ya Klabu ya Simba ni uongozi unaofuata weledi.

Simba ndio mfano wa uongozi kwa klabu nyingine, kwamba wanaendesha mambo yao kwa kufuata utaratibu sahihi kabisa kulingana na ubora wao.

Kweli kikosi chao ni bora, mambo yao yanaonekana yanakwenda kwa utaratibu mzuri kabisa katika kipimo sahihi na kila kitu ni kizuri.


Wengine wanapaswa kuanza kuiga au wameanza kuiga kutokana na wanavyosikia namna ambavyo Simba inaendeshwa. Kitu kizuri ni chachu ya mabadiliko na baadaye mafanikio kwa wengine.

Kwa sasa, mambo yanaanza kwenda tofauti na huenda ikaamka picha mpya kwamba inawezekana hata kwa watu wanaojitambua na kuendesha kazi zao kwa ufasaha kuanza kulumbana hadharani.


Kuna sauti ambayo imeanza kusambaa usiku wa kuamkia juzi, ikisikika Msemaji wa Simba, Haji Manara akimshutumu mambo kadhaa Ofisa Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez.

Maneno ni mengi na inaonekana katika shutuma hizo, Manara analia kudharauliwa, kunyanyaswa na kufanyiwa roho mbaya huku akisisitiza kwamba atazungumza baada ya mechi dhidi ya watani wao wa jadi Yanga kule Kigoma, Jumapili.

Manara ameendelea kueleza anavyokerwa na mambo kadhaa huku akitupa shutuma lukuki kwa Barbara ambaye ameendelea kuwa kimya.


Mchana kwenye ukurasa wake wa Instagram, ameeleza kwamba aliyevujisha sauti ile ni Barbara mwenyewe kwa kuwa yeye ndiye alimtumia. Akasisitiza aliamini anazungumza naye huku akiwa amejipanga kuzungumza baada ya mechi hiyo ya Kigoma, lakini sauti hiyo imevujishwa kwa makusudi.

Hilo ndiyo gumzo kubwa zaidi katika mchezo wa soka, wakati watu wanakwenda katika fainali ya Kombe la Shirikisho mjini Kigoma, sura imekuwa tofauti na sasa ni Manara wa Simba dhidi ya Barbara wa Simba. Jiulize!


Vipi iwe viongozi wa Simba walumbane katika kipindi kama hiki ambacho unatarajia kuiona timu hiyo ikijipanga vizuri kwa ajili ya kushinda mchezo huo?

Kati ya maneno aliyoyazungumza Manara ni kuhusiana na yeye kutuhumiwa kwenda kwenye kambi ya Yanga huku akisisitiza anadhalilishwa na bosi wake huyo ambaye amemuita ni anayependa umaarufu.

Yanga kwao wanaona ni kama hasira za mkizi au vita ya vifaranga vya kuku inayokwenda kuwa faida kwa kunguru au mwewe, jambo ambalo kwa Simba linawapitisha katika sifa mbovu kabisa.


Katika yale maneno, Manara mwisho

alimaliza kwa kumueleza bosi wake huyo

mwanamama “koma”. Lile neno

linalomsisitiza mtu kuacha au kuachana

na jambo fulani. Nami niwasisitize

kwamba iwe hadharani au chinichini,

bado wote hawakupaswa kuonyesheana

nani zaidi kwa kipindi hiki.

Tunamuona Barbara akiwa

amenyamaza, lakini kwa mujibu wa

Manara alimshambulia kwa maneno

kadhaa ambayo yanaonekana kumkera

na kuanzisha mjadala huo ambao binafsi

nauona hauna manufaa kwa Simba kwa

kuwa wao wote wawili ni waajiriwa wa

Simba hata kama ni kweli Barbara


alisema yeye ndiye mwenye Simba kama

alivyosema Manara. Kama viongozi ambacho walipaswa kukiangalia ni maslahi mapana ya kikosi

cha Simba na Wanasimba

wanaoizunguka klabu hiyo. Ikishinda ni

faraja kubwa sana kwao na ikipoteza ni

maumivu makubwa, sasa vipi waingize

jambo linalopoteza mwendo wao

unaopelekea umoja na mafanikio

ambayo yamewapa sifa.

Sifa ya weledi inapotea, sifa ya uongozi

bora kwao inapotea na hata lile jambo la

kushindwa kwamba wanapaswa

kulumbana wakati gani basi ni shida

nyingine kubwa na litakuwa jambo bora


wakikaa kimya, baadaye

wakakutanishwa na ikiwezekana

kuyaweka mambo sawa na waendelee.

Simba inaongozwa na watu ambao ndio

wawakilishi wa kikosi chao. Dhamana

waliyopewa ni kubwa sana, asiwepo

anayeona ni zaidi ya mwingine, asiwepo

atakayeona ni mkubwa kuliko klabu au

bora sana zaidi ya wengine. Ikiendelea

hivyo, watapoteza uelekeo na kuna siku,

watashangaa kuona walipo ni chini ya

wengine.

Kama kuna mgogoro, mazungumzo

hayajawahi kushindwa na kama ni chuki

za mioyo baina yao, basi kuna viongozi

wanaoweza kufanya wakayamaliza lakini

 kwa kilichotokea, badala ya kuishia kwa

Manara au Barbara kinaiangusha Simba

yenyewe kuonekana imefeli kiuongozi.

Wote wawili mkome!



Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: SAWA KOMAA, LAKINI MANARA, BARBARA CHONDE
SAWA KOMAA, LAKINI MANARA, BARBARA CHONDE
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg72qx9P8PlCfWdhNq6hMr_x_gPWOyrmZ_YebGqua-mkYSh1hlZ7tKjq28HnrFPwZgabv0XLDTqYwx5r19d8fwEgXVOZo6rj6rTrkifMADx3CTGezAat-wES52D6YqXnYafWjGpF3CiF18L/w518-h640/hajismanara-202426699_489074115505801_901284282265760485_n.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg72qx9P8PlCfWdhNq6hMr_x_gPWOyrmZ_YebGqua-mkYSh1hlZ7tKjq28HnrFPwZgabv0XLDTqYwx5r19d8fwEgXVOZo6rj6rTrkifMADx3CTGezAat-wES52D6YqXnYafWjGpF3CiF18L/s72-w518-c-h640/hajismanara-202426699_489074115505801_901284282265760485_n.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/07/sawa-komaa-lakini-manara-barbara-chonde.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/07/sawa-komaa-lakini-manara-barbara-chonde.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy