MTEGO WA KUTOKUWA NA UZOEFU UKWEPWE LEO NA KIM MBELE YA MALAWI
HomeMichezo

MTEGO WA KUTOKUWA NA UZOEFU UKWEPWE LEO NA KIM MBELE YA MALAWI

VURUGU za usajili zimeanza taratibu japokuwa usajili wenyewe bado rasmi haujafunguliwa mpaka pale ligi itakapofika tamati. Baadhi ya timu ...

CRISTIANO RONALDO AKAMILISHA MASUALA YA VIPIMO KWA AJILI YA KUJIUNGA NA UNITED
MAKAMBO ANA JAMBO LAKE, MUGALU NAYE PIA NI NDANI YA SPOTI XTRA JUMANNE
VIDEO: MZARAMO AMLIPUA HAJI MANARA

VURUGU za usajili zimeanza taratibu japokuwa usajili wenyewe bado rasmi haujafunguliwa mpaka pale ligi itakapofika tamati. Baadhi ya timu zimeshaonyesha ni sehemu gani ambazo wataenda kusajili pale dirisha likifunguliwa.


Lakini pia kuna wachezaji tayari wameshaanza kufunga mabegi yao wakijiandaa kwenda katika makazi yao mapya ikiwa kwa kuhamia mazima baada ya kukubaliana na timu zao mpya katika vipengele kadhaa.


Yote haya ni mazuri kwa sababu naona msimu ujao wa ligi kuu kutokuwa na muda mrefu kuanza kwake baada ya msimu huu kumalizika, hivyo kuwapata mapema wale ambao mnawataka kutawapunguzia presha lakini pia itatoa muda mzuri kwa wachezaji kuunda  muunganiko wa timu.


Kushindwa au kuchelewa kusajili kutakuwa na athari kubwa sana kwa sababu kama nilivyosema nauona msimu ujao kuanza mapema tofauti na huu hivyo inaweza ligi kuanza kukawa na tatizo la wachezaji kutojuana kwa undani na jinsi wanavyocheza.


Tuliona baadhi ya timu zimefeli msimu huu kwa sababu zilifanya kosa kama hilo la kusajili, wengine walichelewa na wengine walijaza rundo la wachezaji lakini wakajikuta wanaishia pabaya kwa kuwaacha dirisha dogo baada ya kuona hawawezi kuwasaidia hata kidogo.


Mwisho wa yote tunataka kuona usajili ambao utakuwa salama, uliojaa ufundi na usio na mihemko ya namna yoyote ile kwa sababu kama timu itashindwa kufanya namna hiyo basi itakuwa inajichimbia shimo la kutumbukia yenyewe.


Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, leo hii Juni 13 inatarajiwa  kuwa na mechi ya kirafiki ya kimataifa mbele ya Malawi ambayo itapigwa katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar.


Mchezo huu umekuja kwa wakati na upo kwenye ratiba ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) ambapo utakuwa wa kwanza tangu Stars ichukuliwe na kocha Mdenishi Kim Poulsen.


Hii ni mechi muhimu kwa sababu itampa picha Kim ya namna gani kikosi hicho kipo tangu alipoondoka nchini na kurejea, atajua pia  arekebishe wapi na viwango vya wachezaji ambao amewaita ndani ya kikosi hicho atavitambua tu.


Japokuwa ni mchezo ambao unahitaji kutafuta ushindi kwa ajili ya kuongeza pointi kwenye viwango vya dunia vinavyosimamiwa na shirikisho hilo lakini kuna kitu nataka kushauri kidogo.


Ingawa simfundishi Kim pamoja na benchi lake la ufundi nini cha kufanya lakini itapendeza kutoa angalau nafasi kwa wachezaji ambao hawana uzoefu na timu ya taifa kuweza kucheza mechi za namna hii kwa ajili ya kuwajenga zaidi.


Mara kwa mara tumekuwa tukilalamika kuwa wachezaji wengi wa hapa nyumbani hawana uzoefu na mechi za kimataifa hasa pale ambapo tunashiriki michuano ambayo haiwahusishi wachezaji wetu ambao wanacheza soka la kulipwa nje ya nchi.


Hivyo fursa hii iwe kwa wachezaji hao kwa ajili ya kuwajenga na kuwaonesha jinsi wanavyotakiwa kupambana pale ambapo watakapotakiwa kucheza mechi za kimataifa ili baadaye isije kuwa sababu kwamba tumefanya mashindano fulani kwa sababu wachezaji hawana uzoefu.




Credit: SALEH JEMBE

Please subscribe to get all sports news instantly
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: MTEGO WA KUTOKUWA NA UZOEFU UKWEPWE LEO NA KIM MBELE YA MALAWI
MTEGO WA KUTOKUWA NA UZOEFU UKWEPWE LEO NA KIM MBELE YA MALAWI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhYt91QvbuQBWsgSXvvsPjNN9h4UTSkSjmm-i7BSvqmJl-d8dkppuhR4iW-FM25h2BHWcXcP-AEI_CvO1l-fj-LZQQbgIn2GxrLa7kWKNn1ambyof_EgwPHw7PPLwn3velXWajTjasL_UAt/w580-h640/Kim+Poulsen.PNG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhYt91QvbuQBWsgSXvvsPjNN9h4UTSkSjmm-i7BSvqmJl-d8dkppuhR4iW-FM25h2BHWcXcP-AEI_CvO1l-fj-LZQQbgIn2GxrLa7kWKNn1ambyof_EgwPHw7PPLwn3velXWajTjasL_UAt/s72-w580-c-h640/Kim+Poulsen.PNG
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/mtego-wa-kutokuwa-na-uzoefu-ukwepwe-leo.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/06/mtego-wa-kutokuwa-na-uzoefu-ukwepwe-leo.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy