Waziri Mkuu Azitaka TPA, TRA, TASAC NA EGA Zifanye Kazi Kwa Ushirikiano
HomeHabari

Waziri Mkuu Azitaka TPA, TRA, TASAC NA EGA Zifanye Kazi Kwa Ushirikiano

  WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amezitaka Mamlaka ya Mapato Tanzania, Mamlaka ya Bandari Tanzania na Mamlaka ya Serikali Mtandao kufanya k...

 


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amezitaka Mamlaka ya Mapato Tanzania, Mamlaka ya Bandari Tanzania na Mamlaka ya Serikali Mtandao kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuboresha utendaji wa Bandari ya Dar es Salaam

Ameyasema hayo jana(Jumatano, Mei 12, 2021) alipotembelea bandari ya Dar es Salaam ili kuona utendaji wa bandari hiyo.

“TPA endeleeni kuiimarisha bandari yetu, hii ni sura ya uchumi wa nchi yetu, zungumzeni lugha moja ya uwajibikaji, TRA muwepo maeneo yote yanayohitaji uwepo wenu na muda wote wateja wetu wahudumiwe ili bandari yetu iendelee kuwa bora. Nchi nyingi zinatutegemea”

Amesema kuwa Mamlaka ya Mapato Tanzania ihakikishe mfumo wa pamoja wa forodha Tanzania (TANCIS) unafanya kazi kwa ufanisi ili kupuinguza malalamiko ya wateja kuhusu mfumo huo.

“Dosari zote za mfumo wa TANCIS zifanyiwe kazi, mfumo usituharibie, mnapoona kuna madhaifu fanyeni marekebisho ya haraka, tunataka wateja waingie na kutoka kwa muda mfupi” Amesema.

Aidha, Waziri Mkuu amemuagiza Kamishna Mkuu wa TRA apeleke watumishi katika mizani ya TANROADS iliyopo Kurasini Dar es Salam ili kurahisisha ukaguzi wa ‘seal’ pale ambapo magari yamezidisha uzito na yanahitaji kukaguliwa

“TRA kuna foleni kwenye mizani, hakuna watu, kuanzia leo peleka watumishi pale tunataka ukaguzi uwe muda wote”.

Akitolea ufafanuzi kuhusu video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii ya uwepo wa foleni bandarini hapo, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania Eric Hamissi amesema suala hilo halina ukweli na hakuna dereva anayekaa bandarini kwa siku tatu.

“Hata sisi tulishangaa sana kuona ile clip, haina ukweli wowote, dereva Omari Mambo Mei 10, 2021 aliingia saa nane mchana, na ilipofika saa 10.38 alishusha mzigo na kuondoka saa 11.00 jioni”

Aliongeza kuwa kwa sasa asilimia arobaini ya eneo la bandari lipo kwenye ujenzi ikihusisha ujenzi wa njia nne za barabara na ujenzi wa gati namba moja mpaka saba lengo ni kuifanya bandari iweze kuhudumia wateja kwa ufanisi mkubwa “mpaka sasa gati namba moja mpaka tano zimekamilika na gati namba sita na saba zitakamilika mwezi Agosti,2021”

Wakizungumza kwa nyakati tofauti madereva wa malori wanaoingia na kutoka kwenye Bandari ya Dar es Salaam wamesema wanaridhishwa na utendaji kazi wa bandari kwani hawatumii muda mrefu kuingia na kutoka bandarini hapo.

(Mwisho)
IMETOLEWA NA
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Waziri Mkuu Azitaka TPA, TRA, TASAC NA EGA Zifanye Kazi Kwa Ushirikiano
Waziri Mkuu Azitaka TPA, TRA, TASAC NA EGA Zifanye Kazi Kwa Ushirikiano
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEig2XkW0rqW28qtwVhq4O_4NzEbdmVkPK-x2VPAo7i_s3R4N7audGF4OYy7wezIIEvfBv1Mu9pT1wtno0ETvzkEURMmCAhV8nrjnP8-771KdhlnMjt0yRGI-IphQt4e1pFm_YOmoHmZX-Cn/s16000/IMG-20210512-WA0320.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEig2XkW0rqW28qtwVhq4O_4NzEbdmVkPK-x2VPAo7i_s3R4N7audGF4OYy7wezIIEvfBv1Mu9pT1wtno0ETvzkEURMmCAhV8nrjnP8-771KdhlnMjt0yRGI-IphQt4e1pFm_YOmoHmZX-Cn/s72-c/IMG-20210512-WA0320.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/05/waziri-mkuu-azitaka-tpa-tra-tasac-na.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/05/waziri-mkuu-azitaka-tpa-tra-tasac-na.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy