Watu Watano wafikishwa mahakama ya Kisutu kwa kukutwa na meno ya tembo
HomeHabari

Watu Watano wafikishwa mahakama ya Kisutu kwa kukutwa na meno ya tembo

Watu watano wakazi wa Mkoa wa Katavi na Rukwa wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka mawili likiwem...

Matanki ya kuhifadhi mafuta yachomwa moto Libya
Cameroon Reclaims Military Base From Boko Haram
7 dead, 414 rescued after fire cripples Greek ferry in Adriatic Sea


Watu watano wakazi wa Mkoa wa Katavi na Rukwa wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na mashtaka mawili likiwemo la kukutwa na vipande vinne vya meno ya tembo vyenye thamani ya Sh34.6 milioni.

Washtakiwa hao waliosomewa mashtaka yao na wakili wa Serikali mwandamizi, Wankyo Saimon mbele ya Hakimu Mkazi mwandamizi, Kassian Matembele ni Craft Kileo, Godfrey Kashuli, Richard Kafwa, Moses Zakaria na Benjamin Lushina.

Kabla ya kusomewa mashtaka yao, Matembele aliwaeleza kuwa hawatakiwi kujibu chochote kwa sababu mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kusikiliza kesi ya uhujumu uchumi.

Akiwasomea mashtaka yao, Simon amedai katika shtaka la kwanza linalomkabili Kileo na Kashuli inadaiwa Mei 5, 2021 wakiwa eneo la Ukonga Wilaya ya Ilala walikutwa na vipande vinne vya meno ya tembo ambavyo ni mali ya Serikali bila kuwa na kibali cha mkurugenzi wa wanyamapori.

Katika shtaka la pili linalowakabili washtakiwa wote inadaiwa kati ya Aprili Mosi, 2021 na Mei 5, 2021 wakiwa eneo la Katavi na Dar es Salaam walisafirisha vipande vinne vya meno hayo bila kibali cha mkurugenzi huyo.

Baada ya kusomewa mashtaka yanayowakabili, Matembele aliwaeleza kuwa mahakama hiyo haiwezi kuwapa dhamana kwa sababu sheria inaeleza kuwa thamani ya mali ikizidi Sh10 milioni, dhamana inatolewa na mahakama kuu, kwamba kama wanataka dhamana wakaombe katika mahakama hiyo.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Juni 8, 2021 na washtakiwa wamerudishwa rumande.




Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Watu Watano wafikishwa mahakama ya Kisutu kwa kukutwa na meno ya tembo
Watu Watano wafikishwa mahakama ya Kisutu kwa kukutwa na meno ya tembo
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgYJImi4tBCo1A1X5wVsq8VO_Rz8pTCsDfnvj0cNig0PJ8KfLh8ksGU0dAN1v70yQbkSSd8McEfFRcYyV4y4vm2SHXtj4uXAInJr4MZ9zrx3OPnT5JyabmiiPFFvl-2a_AGRHdfW0idUAgs/s16000/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgYJImi4tBCo1A1X5wVsq8VO_Rz8pTCsDfnvj0cNig0PJ8KfLh8ksGU0dAN1v70yQbkSSd8McEfFRcYyV4y4vm2SHXtj4uXAInJr4MZ9zrx3OPnT5JyabmiiPFFvl-2a_AGRHdfW0idUAgs/s72-c/1.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/05/watu-watano-wafikishwa-mahakama-ya.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/05/watu-watano-wafikishwa-mahakama-ya.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy