Viongozi Mbalimbali Wamlilia Rais Magufuli
HomeHabari

Viongozi Mbalimbali Wamlilia Rais Magufuli

Viongozi mbalimbali wa kisiasa wametoa salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Rais John Magufuli kilichotokea Machi 17, 2021 katika Hosp...

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo July 1
Bashe Aagiza Ras Tabora Kuwaondoa Watumishi Wa Manispaa Ya Tabora Waliochukua Mashamba Katika Mashamba Katika Skimu Inala
Makamu Wa Rais Dkt.Mpango Awasili Nchini Ufaransa Kuhudhuria Jukwaa La Kizazi Chenye Usawa


Viongozi mbalimbali wa kisiasa wametoa salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Rais John Magufuli kilichotokea Machi 17, 2021 katika Hospitali ya Mzena jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan ametangaza kifo cha Rais Magufuli saa tano usiku wa kuamkia leo  akisema kimetokana na tatizo la moyo la mfumo wa umeme ambalo alikuwa nalo kwa zaidi ya miaka 10.

Katika ukurasa wake wa Twitter, Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi ameandika, “kwa masikitiko makubwa Machi 17, 2021 saa 12 jioni tumempoteza Rais John Magufuli ambaye amefariki kwa maradhi ya moyo katika Hospitali ya Mzena jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.”

Kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe naye ametoa salamu zake za rambirambi akieleza kupokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Rais Magufuli huku akitoa pole kwa mama Janeth Magufuli pamoja na familia yake.

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa naye ameandika katika ukurasa wake wa Twitter: “Bwana alitoa na Bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe. Amina.”
 
Wengine waliotoa salamu za Pole ni Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson,Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Felix Tshisekedi,Rais wa Somalia Mohamed Farmaajo,Rais wa Venezuela Nicolás Maduro 

Mbali na salamu hizo za watu mbalimbali, vyombo vya habari vya ndani na nje ya nchi vimeripoti taarifa ya kifo

Rais Magufuli amefariki akiwa na umri wa miaka 61 akiwa ametawala kwa miaka karibu sita tangu alipochaguliwa katika uchaguzi wa Oktoba 2015. Pia, alishinda uchaguzi wa Oktoba 28 mwaka jana kwa muhula wake wa pili ambao hajaumaliza.

Mama Samia ametangaza siku 14 za maombolezo ya kifo chake ambapo bendera zitapepea nusu mlingoti wakati taratibu za mazishi zikiandaliwa.



Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Viongozi Mbalimbali Wamlilia Rais Magufuli
Viongozi Mbalimbali Wamlilia Rais Magufuli
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj3l8ZFvZZm2OGa6Ds3bXDidfSDpegBUf9cwRdEj3_aGZcKuDfM26Aw0yR2geKM4vO9rKN5sr4cdqF1b859xq-4kRmTAxFW58pOWPVSx0g0SHQHdOz8Q4hyphenhyphenCQf5VgPRRl2Nt7x_qTnAqiy4/s16000/1.png
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj3l8ZFvZZm2OGa6Ds3bXDidfSDpegBUf9cwRdEj3_aGZcKuDfM26Aw0yR2geKM4vO9rKN5sr4cdqF1b859xq-4kRmTAxFW58pOWPVSx0g0SHQHdOz8Q4hyphenhyphenCQf5VgPRRl2Nt7x_qTnAqiy4/s72-c/1.png
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/03/viongozi-mbalimbali-wamlilia-rais.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/03/viongozi-mbalimbali-wamlilia-rais.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy