Marekani kutoa tamko kuhusu Saudi Arabia kuhusiana na mauaji ya muandishi habari Jamal Khashoggi.
HomeHabari

Marekani kutoa tamko kuhusu Saudi Arabia kuhusiana na mauaji ya muandishi habari Jamal Khashoggi.

Serikali ya Marekani inatarajia leo Jumatatu kutoa tamko kuhusu Saudi Arabia kufuatia ripoti ya kijasusi ya Marekani kusema kuwa mrithi w...


Serikali ya Marekani inatarajia leo Jumatatu kutoa tamko kuhusu Saudi Arabia kufuatia ripoti ya kijasusi ya Marekani kusema kuwa mrithi wa kiti cha ufalme wa taifa hilo Mohammed Bin Salman aliamuru mauaji ya muandishi habari Jamal Khashoggi.

Rais wa Marekani Joe Biden, mwishoni mwa wiki iliyopita, alisema atatangaza Jumatatu wiki hii hatua watakayochukua kwa Saudi Arabia.

Utawala wa Biden umekosolewa hasa katika ripoti ya gazeti la Washington Post iliyosema Biden angeonesha nguvu zake kwa Mohammed Bin Salman ambaye hakuwekewa vikwazo vya aina yoyote licha ya kutajwa kuhusika na mauaji ya Khashoggi.

Wiki iliyopita Saudi Arabia ilifutilia mbali madai ya kumhusisha Mohammed Bin Salman Bin Salman na kifo cha Khashoggi yalitolewa katika ripoti ya kijasusi iliyotolewa na Marekani ikifichua kuwa Mwana mfalme huyo aliidhinisha mauaji ya mwandishi habari Jamal Khashoggi mwaka 2018.

Hapo kabla Saudi Arabia ilisema mauaji ya Khashoggi kwenye ubalozi mdogo wa Saudi Arabia nchini Uturuki yalifanywa katika operesheni ya kihalifu na kukanusha kuhusika kwa mwanamfalme Salman.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Antony Blinken alisema Washington inalenga kuchukua mwelekeo mpya wa kisera lakini siyo kuvuruga mahusiano yake na Saudi Arabia ambayo ni mshirika wa karibu wa usalama kwenye eneo la Mashariki ya Kati.

Mwandishi huyo aliyekuwa na umri wa miaka 59 wakati wa mauaji yake, aliambiwa na balozi wa Saudia afike katika ubalozi wa taifa hilo mjini Istanbul, ili kupata nyaraka kadhaa alizohitaji ili aweze kufunga ndoa na mpenzi wake raia wa Uturuki, Hatice Cengiz.




Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Marekani kutoa tamko kuhusu Saudi Arabia kuhusiana na mauaji ya muandishi habari Jamal Khashoggi.
Marekani kutoa tamko kuhusu Saudi Arabia kuhusiana na mauaji ya muandishi habari Jamal Khashoggi.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjvAfojdSoG4GeOIWFe737VMpUcmMtjPhOdf_u7DegcKIYpBnkbu4g_ERnHGJezhF8MEoxvUVG4BsblU0f5tVaURHJ8lpDGTHQeVaG5jKLqDksEq__uVdN1M6LgAI8RNXa_bpxfXdtrPFWY/s16000/1.webp
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjvAfojdSoG4GeOIWFe737VMpUcmMtjPhOdf_u7DegcKIYpBnkbu4g_ERnHGJezhF8MEoxvUVG4BsblU0f5tVaURHJ8lpDGTHQeVaG5jKLqDksEq__uVdN1M6LgAI8RNXa_bpxfXdtrPFWY/s72-c/1.webp
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/03/marekani-kutoa-tamko-kuhusu-saudi.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/03/marekani-kutoa-tamko-kuhusu-saudi.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy