Kamati Ya Bunge Ya Miundombinu Yatembelea Ofisi Za Ttcl Jijini Dar Es Salaam
HomeHabari

Kamati Ya Bunge Ya Miundombinu Yatembelea Ofisi Za Ttcl Jijini Dar Es Salaam

 Na Debora Sanja, Bunge Kamati ya Bunge ya Miundombinu imeitaka Serikali kupitia Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kuweka ms...

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya leo August 1
Naibu Waziri Kundo Amtumbua Meneja Wa TTCL Kagera, Shirika La Posta Kagera Kuchunguzwa
Mhandisi Masauni Aridhishwa Na Utendaji Wa Shirika La Bima La Taifa


 Na Debora Sanja, Bunge
Kamati ya Bunge ya Miundombinu imeitaka Serikali kupitia Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kuweka msukumo wa kudai madeni ambayo Shirika la Mawasiliano (TTCL) na Shirika la Posta linawadai wateja wake.

Wito huo umetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mheshimiwa Moshi Kakoso wakati Kamati ilipotembelea ofisi za TTCL Jijini Dar es Salaam.

Alisema madeni yote sugu yakianza kulipwa yatasaidia mashirika hayo kufanya kazi kwa ufanisi ikiwa ni pamoja na kujiendesha kibiashara.

“Haya madeni ambayo TTCL na Shirika la Posta wanawadai wateja wao yakianza kulipwa yataleta manufaa makubwa kwa mashirika haya kwa kuwa yataweza kujiendesha kibiashara,” alisema.

Aidha, aliipongeza Serikali kwa kulisaidia Shirika la Posta kwa kulipunguzia changamoto mbalimbali ikiwemo kuwaondolea baadhi ya madeni ili liweze kujiendeleza.

Aliitaka pia Serikali  kuangalia uwezekano wa kuwapatia magari Shirika hilo la Posta ili liweze kusimama vizuri.

Mheshimiwa Kakoso pia alimpongeza Waziri wa Mawasiliano na Teknojia ya Habari Mheshimiwa Faustine Ndugulile kwa kazi nzuri aliyoifanya ya kusimamia sekta ya mawasiliano ndani ya kipindi kifupi.

“Natoa pongezi sana kwa kazi nzuri, endelea kuzisimamia taasisi zako vizuri na kazi yako itaonekana, ” alisema.

Alisema Kamati ipo tayari kushirikiana na Wizara yake na kwamba kama kuna kikwazo chochote kinachohitaji mabadiliko ya sheria wasisite kupeleka mapendekezo Bungeni.

Kwa upande wake Mheshimiwa Ndugulile aliishukuru Kamati kwa ziara hiyo na kuahidi kushirikiana kwa karibu ikiwemo kuyafanyia kazi maelekezo yote ambayo Kamati imeyatoa.

Kamati ya Miundombini mbali na kutembelea Ofisi za TTCL na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na kupokea taarifa za utekelezaji wa majukumu yao pia ilipokea taarifa ya Shirika la Posta na Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF)


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Kamati Ya Bunge Ya Miundombinu Yatembelea Ofisi Za Ttcl Jijini Dar Es Salaam
Kamati Ya Bunge Ya Miundombinu Yatembelea Ofisi Za Ttcl Jijini Dar Es Salaam
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhS8E4TEZatOd2kdmD2ANVBoF6gDKxRyRNXtstgr4tKZYAA2dJ9XDrlVGNJhPU5oxCmu6cpWQ-35e74ok9G2Kx6FM1mhVeYisySzJZdkfKqpvyNbxvdJaSO8mE9iQJiQlz-nJ_-UlqR4Wfq/s16000/1.jpeg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhS8E4TEZatOd2kdmD2ANVBoF6gDKxRyRNXtstgr4tKZYAA2dJ9XDrlVGNJhPU5oxCmu6cpWQ-35e74ok9G2Kx6FM1mhVeYisySzJZdkfKqpvyNbxvdJaSO8mE9iQJiQlz-nJ_-UlqR4Wfq/s72-c/1.jpeg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/03/kamati-ya-bunge-ya-miundombinu.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/03/kamati-ya-bunge-ya-miundombinu.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy