Rais Magufuli: Serikali haijazuia matumizi ya barakoa
HomeHabari

Rais Magufuli: Serikali haijazuia matumizi ya barakoa

 Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli leo ameungana na Waumini wa Parokia ya Mtakatifu Petro, Oysterbay Jij...


 Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli leo ameungana na Waumini wa Parokia ya Mtakatifu Petro, Oysterbay Jijini Dar es Salaam kusali Misa Takatifu ya Jumapili (Dominika ya 1 ya Kwaresma) na amewashukuru Watanzania kupitia Madhehebu yao ya Dini kwa kuitikia wito wa maombi na kufunga ili Mungu aepushe ugonjwa wa Korona unaosababisha vifo vya watu duniani.

Rais Magufuli amesema Wakristo ambao wapo katika kipindi cha Kwaresma na Waislamu ambao wanakaribia kuingia katika kipindi cha mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, waendelee kumuomba Mungu kwani pamoja na jitihada za kibinadamu za kukabiliana na ugonjwa huo, Mungu ndiye muweza wa yote na husimama kwa kila jambo.


Amewataka Watanzania kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa Korona kama zinavyoelekezwa na Wataalamu wa afya na amefafanua kuwa Serikali haijazuia matumizi ya barakoa katika kujikinga kuambukizwa virusi vya Korona bali Watanzania wachukue tahadhari kwa kutumia barakoa zinazotengezwa hapa nchini zikiwemo za Bodi ya Dawa (MSD) au zinazotengezwa na Watanzania wenyewe kwa kuwa barakoa zinazoingizwa kutoka nje ya nchi zina mashaka ya kuwa sio salama.

Aidha, Rais Magufuli amesisitiza kutumia njia za asili za kukabiliana na magonjwa ya kupumua ukiwemo ugonjwa huo ikiwa ni pamoja na kujifukiza (kupiga nyungu).

Rais Magufuli amewataka Watanzania kuondoa hofu inayopandikizwa ambayo ina madhara zaidi, na amesisitiza kuendelea kumtumaini na kumtanguliza Mwenyezi Mungu kwa kuwa njia za kujikinga kwa barakoa, kutogusana na kutokaribiana (social distancing) pamoja na kujifungia majumbani (lockdown) vimeonekana kutokuwa suluhisho la uhakika kwani Mataifa yanayofanya hivyo watu wake wanapoteza maisha kwa maelfu ikilinganishwa na hapa Tanzania.

Amempongeza Paroko wa Parokia ya Mtakatifu Petro, Oysterbay Padre Dkt. Alister Makubi kwa mahubiri yaliyoeleza namna Yesu alivyojaribiwa na kwamba hata changamoto za sasa ikiwemo ugonjwa wa Korona ni majaribu ambayo yatapita


.


Credit: MPEKUZI

Thanks for your time please share with your friends
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Rais Magufuli: Serikali haijazuia matumizi ya barakoa
Rais Magufuli: Serikali haijazuia matumizi ya barakoa
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj6fQ3cSBD2yZzWD7pbqH3EoT8gYTmEm0sjBJrngC1jMP0CK1cvfezfuaSem7G98uPjNSrSwk2RtHIGh1G0HMHl1FRpy31uqSOcwP0riJS50USMdfes8RpQDBC5fEfaEip1vm3ELvlmfwiT/s16000/k8-1-660x400.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj6fQ3cSBD2yZzWD7pbqH3EoT8gYTmEm0sjBJrngC1jMP0CK1cvfezfuaSem7G98uPjNSrSwk2RtHIGh1G0HMHl1FRpy31uqSOcwP0riJS50USMdfes8RpQDBC5fEfaEip1vm3ELvlmfwiT/s72-c/k8-1-660x400.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/rais-magufuli-serikali-haijazuia.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2021/02/rais-magufuli-serikali-haijazuia.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy