KLABU ya Azam itakuwa nje ya uwanja wake wa nyumbani ‘Azam Complex’ kwa takribani mwezi mmoja ikicheza mechi za ugenini. Akizungumza na g...
KLABU
ya Azam itakuwa nje ya uwanja wake wa nyumbani ‘Azam Complex’ kwa
takribani mwezi mmoja ikicheza mechi za ugenini. Akizungumza na gazeti
hili jana msemaji wa Azam, Jaffa Idd alisema mchezo wa mwisho kwa Azam
kucheza nyumbani ni ule dhidi ya Mwadui Februari 7 ambapo ilishinda bao
1-0.
“Timu itakuwa ugenini kucheza mechi tano, kati ya hizo nne ni za Ligi Kuu Tanzania Bara na mmoja wa kombe la Shirikisho dhidi ya Panone FC ya mkoani Kilimanjaro,” alisema Idd.
Azam FC ilianza kucheza mchezo wa kwanza ugenini dhidi ya Coastal Union ya Tanga jana katika Uwanja wa Mkwakwani Tanga kisha itakwenda Mbeya kucheza na Mbeya City, Februari 20 na itasalia hapo kucheza na Prisons Februari 24.
Baada ya kumaliza kibarua chake hicho, itaelekea moja kwa moja Moshi, Kilimanjaro kumenyana na Panone katika mchezo wa raundi ya 16 bora ya michuano ya Kombe la Shirikisho utakaofanyika Uwanja wa Ushirika Februari 28, 2016.
Baada ya kurejea Dar es Salaam itapumzika kwa siku sita na Machi 5, itashuka kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuvaana na wenyeji wao, Yanga mchezo ambao ni kiporo.
“Timu itakuwa ugenini kucheza mechi tano, kati ya hizo nne ni za Ligi Kuu Tanzania Bara na mmoja wa kombe la Shirikisho dhidi ya Panone FC ya mkoani Kilimanjaro,” alisema Idd.
Azam FC ilianza kucheza mchezo wa kwanza ugenini dhidi ya Coastal Union ya Tanga jana katika Uwanja wa Mkwakwani Tanga kisha itakwenda Mbeya kucheza na Mbeya City, Februari 20 na itasalia hapo kucheza na Prisons Februari 24.
Baada ya kumaliza kibarua chake hicho, itaelekea moja kwa moja Moshi, Kilimanjaro kumenyana na Panone katika mchezo wa raundi ya 16 bora ya michuano ya Kombe la Shirikisho utakaofanyika Uwanja wa Ushirika Februari 28, 2016.
Baada ya kurejea Dar es Salaam itapumzika kwa siku sita na Machi 5, itashuka kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuvaana na wenyeji wao, Yanga mchezo ambao ni kiporo.
COMMENTS