Uenyekiti wa Mrema wapingwa mahakamani
Homekisiasa

Uenyekiti wa Mrema wapingwa mahakamani

Mwenyekiti wa Taifa wa chama cha TLP , Augustine Mrema   Mwasisi wa chama cha TLP, Stanley Nda...





Mwenyekiti wa Taifa wa chama cha TLP , Augustine Mrema  
Mwasisi wa chama cha TLP, Stanley Ndamugoba amemburuza mahakamani Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, Augustine Mrema akidai si kiongozi halali.
Kesi hiyo ya madai namba 33/2015 ilifunguliwa na Ndamugoba Ijumaa iliyopita katika Mahakama Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam ikiambatanishwa na hati ya usikilizwaji wa haraka.
Katika kesi hiyo ambayo Baraza la Wadhamini limeunganishwa kama mdaiwa wa pili, Ndamugoba ameiomba mahakama itamke uongozi wa Mrema ulifikia kikomo mwaka mmoja uliopita. Mdai anaiomba mahakama kuu itamke kuwa kwa vile muda wake wa uongozi ulimalizika mwaka mmoja uliopita, Mrema hana mamlaka ya kuitisha mkutano mkuu wa uchaguzi.
Ndamugoba mwenyewe alilithibitishia gazeti hili jana kufungua kesi hiyo akisema leo atakwenda Mahakama Kuu ili kuchukua samansi za kumuita Mrema shaurini pamoja na Baraza la Wadhamini.
“Ni kweli nimefungua kesi na nafikiri kesho (leo) samansi zitatoka,” alisema.
Hata hivyo Mrema alipoulizwa na gazeti hili jana kuhusu kuwapo kwa kesi hiyo, alisema yeye hakujiongezea muda kwa nguvu bali katiba ya TLP ndiyo ilimwongezea muda huo.
“Mimi sikujiongezea muda kwa nguvu wala sikuongezewa na mtu yeyote. Sisi tunafuata katiba ya TLP. Tatizo hapa ninaloliona ni vita ya ubunge Jimbo la Vunjo,” alisema Mrema.
Mrema alifafanua kuwa kamati kuu iliyopita, ilifanya uamuzi na kumpitisha yeye kuwa mgombea ubunge Jimbo la Vunjo na mgombea pekee wa nafasi ya uenyekiti wa TLP Taifa.
Bila kutaja kifungu cha katiba, Mrema alisema halmashauri kuu ya TLP imetoa madaraka kwa kamati kuu kufanya kazi kwa niaba yake na mkutano mkuu wa TLP.
“Katiba iko wazi kwamba endapo kuna mazingira yatajitokeza, kamati kuu imepewa mamlaka ya kufanya kazi za halmashauri kuu na mkutano mkuu na uamuzi huu ulifikiwa 2007,” alisema. “Tulitumia kipengele hicho kusogeza mbele mkutano mkuu wa uchaguzi kwa mwaka mmoja na tumeshatangaza mkutano mkuu wa uchaguzi utafanyika Aprili 23, mwaka huu,” alisisitiza.
Mrema alisema maelezo hayo ndiyo ambayo waliyatoa pia kwa Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi baada ya baadhi ya wanachama kulalamika na huo ndiyo msimamo wa kikatiba
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Uenyekiti wa Mrema wapingwa mahakamani
Uenyekiti wa Mrema wapingwa mahakamani
http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/2646700/highRes/961663/-/maxw/600/-/pdmumhz/-/mrema.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/03/uenyekiti-wa-mrema-wapingwa-mahakamani.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/03/uenyekiti-wa-mrema-wapingwa-mahakamani.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy