Mshukiwa wa Al Shabab akamatwa Kenya
HomeHabariKimataifa

Mshukiwa wa Al Shabab akamatwa Kenya

Mshukiwa mmoja wa kundi la wapiganaji wa Al Shaabab amekamatwa kufuatia shambulizi la kigaidi Kaskazini mwa Kenya Mshukiwa mmoja amekamatw...



Mshukiwa mmoja wa kundi la wapiganaji wa Al Shaabab amekamatwa kufuatia shambulizi la kigaidi Kaskazini mwa Kenya

Mshukiwa mmoja amekamatwa na polisi kufuatia shambulio la kigaidi lililotokea mjini Mandera kaskazini mwa Kenya siku ya Jumapili usiku, na kusababisha kifo cha mtu mmoja na wengine kadhaa kujeruhiwa.

Idara ya polisi nchini Kenya imesema kuwa mshukiwa huyo alinaswa na maafisa wa polisi na jeshi waliokuwa wakiwasaka washukiwa waliotekeleza shambulio hilo.

Mwandishi wa BBC Robert Kiptoo anasema kuwa Inspekta generali wa polisi nchini Kenya, Joseph Boinet amemdhibitishia kukamatwa kwa mshukiwa huyo, kufuatia shambulizi hilo mjini Mandera.

Akizungumza wakati alipowatembelea maafisa wa polisi na raia waliojeruhiwa kwenye shambulizi lingine lililotokea siku ya Ijumaa mjini Mandera.



 
Al Shabab inataka majeshi ya Kenya kuondoka nchini Somalia

Boinet, amesema operesheni inayojumuisha maafia wa jeshi la polisi inaendelea katika sehemu hiyo na kuwa hali ya usalama kwa sasa ni tulivu.

Shambulio hilo lilitokea siku mbili tu baada ya msafara wa gavana wa jimbo hilo kuvamiwa na wanamgambo wa kiislamu kutoka Somalia wa Al shabaab.

Watu watatu waliuawa wakiwemo maafisa wawili wa polisi.

Na katika shambulio la jana ripoti zinasema watu waliokuwa kwenye gari walianza kuwamiminia risasi raia waliokuwa wakinunua vitu katika duka moja, kabla ya kutoweka.





Inspekta generali wa polis nchini Kenya, Joseph Boinet alichukua hatamu juma lililopita



Mmoja wao alifariki papo hapo huku wengine waliojeruhiwa kwa risasi wanaendelea kupokea matibabu katika hospitali moja mjini Mandera.

Kundi hilo la Kiislamu lenya uhusiano na kundi la kigaidi la Al Qaeda limefanya mashambulio kadhaa nchini kenya, tangu wanajeshi wa Kenya walipotumwa nchini humo kuangamiza kundi hilo.

Aidha wamedai kuwa wataendelea mashambulio dhidi ya Kenya hadi kenya itakapoondoa majeshi yake nchini humo.

Lakini serikali ya Kenya imekariri kuwa wanajeshi wake watasalia nchini humo hadi pale kundi hilo litakapotokomezwa kabisa.
 
>>>BBC
Mshirikishe rafiki yako hapo chini tafadhali
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Mshukiwa wa Al Shabab akamatwa Kenya
Mshukiwa wa Al Shabab akamatwa Kenya
http://ichef.bbci.co.uk/news/ws/660/amz/worldservice/live/assets/images/2014/12/10/141210184431_jihadists_al_shabab_624x351_ap.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/03/mshukiwa-wa-al-shabab-akamatwa-kenya.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/03/mshukiwa-wa-al-shabab-akamatwa-kenya.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy