Sumatra yafungia mabasi mawili
HomeHabariKitaifa

Sumatra yafungia mabasi mawili

MAMLAKA ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), imefungia mabasi mawili ya Kampuni ya Ibra Line Limited, yanayofanya safari za D...






MAMLAKA ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), imefungia mabasi mawili ya Kampuni ya Ibra Line Limited, yanayofanya safari za Dar es Salaam-Arusha na Moshi-Arusha, kwa kutoza nauli zaidi, kuongeza na kufupisha ruti kinyemela.

Mabasi hayo; T 288 CBV linalosafirisha abiria kutoka Arusha kwenda Dar es Salaam na T 843 BVF linalofanya safari zake kati ya Moshi na Arusha, yamezuiwa kusafirisha abiria kwa siku 30, kuanzia leo.

Akizungumza na gazeti hili Dar es Salaam jana, Meneja Leseni wa Sumatra, Leo Ngowi, alisema adhabu hiyo ni fundisho kwa wamiliki na wafanyakazi wa mabasi yenye leseni ya kusafirisha abiria, wanaokiuka masharti ya leseni hiyo kwa visingizio mbalimbali.

Kwa mujibu wa Ngowi, ukaguzi uliofanywa na maofisa wa mamlaka hiyo, kwa ushirikiano na polisi katika Kituo Kikuu cha Mabasi mjini Moshi, Januari 7, mwaka huu, umebaini kuwa, basi namba T288 CBV lilikatisha ruti na kuanzia safari yake ya siku hiyo mjini Moshi badala ya Arusha kwenda Dar es Salaam.

“Kwa maana hiyo, basi hilo liliwanyima haki ya kusafiri abiria waliokuwa Arusha wakitaka usafiri wa kwenda Dar es Salaam. Pia, wahusika katika basi hilo waliwatoza abiria nauli ya Sh 35,000 kutoka Moshi kwenda Dar es Salaam, badala ya Sh 28,500 kwa njia hiyo,” Ngowi alisema na kueleza kuwa hayo ni makosa yanayostahili adhabu iliyotolewa.

Mbali na makosa hayo, Ngowi alisema kuwa, wahusika katika basi hilo, waliandika taarifa za uongo kwenye tiketi walizowapa abiria kuwa wamewatoza nauli ya Sh 28,500 iliyoidhinishwa na Sumatra wakati waliwatoza Sh 7,000 zaidi ya iliyopangwa na mamlaka hiyo.

“Abiria waliokuwa katika mabasi yote mawili, walibughudhiwa kwa kutolewa lugha chafu siku hiyo, ambapo walitoa ushirikiano kwa kuwafahamisha ukweli maofisa waliokuwa wakifanya ukaguzi kituoni hapo, jambo lililosababisha wahusika watuhumiwe chini ya kifungu namba 18 (1) (a), cha masharti ya leseni ya usafirishaji abiria ya mwaka 2007,” alisema.
Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Sumatra yafungia mabasi mawili
Sumatra yafungia mabasi mawili
http://www.habarileo.co.tz/images/ibra-line.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/sumatra-yafungia-mabasi-mawili.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/sumatra-yafungia-mabasi-mawili.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy