Simbachawene ashikilia msimamo wa Muhongo
Rais Jakaya Kikwete akimwapisha, George Simbachawene kuwa Waziri wa Nishati na Madini Ikulu jijini Dar es Salaam jana.
HomeHabariKitaifa

Simbachawene ashikilia msimamo wa Muhongo

Rais Jakaya Kikwete akimwapisha, George Simbachawene kuwa Waziri wa Nishati na Madini Ikulu jijini Dar es Salaam jana. WAZIRI mpya wa...



WAZIRI mpya wa Nishati na Madini, George Simbachawene, amesema ni vigumu kupata mwekezaji mzawa katika kazi za uchimbaji wa gesi, kwa kuwa kazi hiyo ni gharama kubwa duniani na kampuni za uchimbaji gesi hazizidi kumi.

Akizungumza na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kuapishwa kushika wadhifa huo na Rais Jakaya Kikwete Ikulu Dar es Salaam jana, Simbachawene alisema kauli kwamba wazawa hawawezi kuwekeza katika gesi, iliyotolewa na aliyemtangulia, Profesa Sospeter Muhongo, haikueleweka vizuri.

Alifafanua kuwa Watanzania wanaweza kuwekeza katika nyanja ya utoaji huduma kwa wachimbaji wa gesi na kuongeza kuwa mpaka sasa kuna maeneo ya huduma ambayo Watanzania wangeweza kuwekeza, lakini hawajafanya hivyo.

“Kuhusu kutoa vitalu kwa Watanzania kila mtu angependa kupewa kitalu cha gesi. Ukipata kitalu ndio umeshatoka, hata mimi ningependa kupata kimoja halafu nikitoka nakwenda Huston (Marekani) na kukiuza na kutoka,” alisema.

Alisema la msingi ni kuhakikisha mikataba ya uchimbaji gesi, inanufaisha Watanzania wote na katika kutoa huduma kwa wachimbaji, atapigania Watanzania wapate fursa ya kuwekeza huko. Alisisitiza umuhimu wa kushirikiana na sekta binafsi na kuongeza kuwa lakini katika ushirikiano huo, lazima kuwepo na uwiano kati ya ushirikiano na maendeleo ya wananchi.

Kuhusu jukumu la kusambaa umeme, Simbachawene alisema atachukua Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kuanza nayo, ili kuhakikisha mafanikio ya usambazaji umeme yaliyopatikana chini ya uongozi wa Profesa Muhongo, yanaendelezwa na hatimaye Watanzania wote wapate umeme.

Naye Waziri mpya wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, amesema anajua Watanzania wengi wanateseka kwa kunyang’anywa ardhi katika maeneo mbalimbali na hasa Dar es Salaam.

Amesema kwa kuwa amewahi kufanya kazi katika jiji la Dar es Salaam, ambako alikuwa Mkuu wa Mkoa, anajua hali ya unyanyasaji katika ardhi ilivyo na kuwataka Watanzania wenye matatizo na ardhi, kutoa taarifa ili wasaidiwe.

Lukuvi alikiri kukabiliwa na changamoto ya baadhi ya watendaji wasio waaminifu katika sekta hiyo na kuongeza atajitahidi kukabiliana na changamoto hiyo kwa uaminifu.

Name

Afya,4,Ajira,2657,Audio,26,Biashara,2,Burudani,43,Economics,1,ELIMU,26,Gossip,38,Habari,3618,History,2,Kimataifa,202,kisiasa,13,Kiswahili,6,Kitaifa,147,Magazeti,44,Matokeo,3,Matukio,89,Michezo,2829,Muziki,62,Nairobi aiport,1,Ripoti,4,Tools,1,Top Stories,757,Video,47,Vituko,15,
ltr
item
Antagon Blog: Simbachawene ashikilia msimamo wa Muhongo
Simbachawene ashikilia msimamo wa Muhongo
http://www.habarileo.co.tz/images/resized/images/kiapo_chawene_300_174.jpg
Antagon Blog
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/simbachawene-ashikilia-msimamo-wa.html
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/
https://antagonf.blogspot.com/2015/01/simbachawene-ashikilia-msimamo-wa.html
true
8268252095325502418
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy